Wednesday, April 20, 2016

RAIS WA ZANZIBAR, DKT. SHEIN ATEMBELEA KAMBI YA KIPINDUPINDU

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Daktari dhamana wa Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu Ramadhan Mikidadi Suleiman leo asubuhi alipotembelea kituoni hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja,wengine ni Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo(wa pili kushoto) na naibu Waziri wa Wizara hiyo Harusi Said Suleiman na Katibu Mkuu Dkt.Juma Malik Akili (katikati).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipata maelezo kutoka Mkurugenzi kinga Wizara ya Afya Dk.Mohamed Dahoma (katikati) wakati alipotembelea Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja leo asubuhi,wengine ni Daktari dhamana wa Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu Ramadhan Mikidadi Suleiman (kushoto)Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt.Jama Adam Taib(wa pili kushoto).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa maelezo kwa Uongozi wa Wizara ya Afya wakati alipotembelea Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja leo asubuhi,(wa pili kushoto) Waziri wa Afya Mahmoud Thabiti Kombo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akimsikiliza Mwanamama Siti Akida Makame mkaazi wa Ziwa Maboga aliyeruhusiwa kurudi nyumbani katika kituo cha Maradhi ya Kipindupindu hapo Chumbuni Karakana Wilaya ya Magharibi Unguja,baada ya kuugua maradhi hayo wakati Rais alipotembelea Kituo hicho leo asubuhi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Mkuu wa Shirika la Kimataifa la LIONS CLUBS Kanda ya Tanzania na Uganda Bw.Hyderall Gangji wakati alipotembelea Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja leo asubuhi,wengine (kushoto) Mustafa kudrati LIONS CLUBS Tanzania na Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo.
Baadahi ya watoa huduma na wananchi wakisubiri huduma katika Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu kama wanavyoonekwanwa wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipotembelea kituoni hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja leo asubuhi.Picha na Ikulu.

No comments: