Tuesday, April 26, 2016

MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA ELIMU TANZANIA AZUNGUMZA NA WANAFUNZI SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA WERUWERU

Mgeni rasmi katika mahafali ya 31 ya kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Wasichana ya Weruweru ,Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania ,Joel Raulent akitoa hotuba yake wakati wa mahafali hayo.
Mgeni rasmi katika mahafali hayo,Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania,Joel Raulent akitunuku vyeti kwa wahitimu 390 wa kidato cha sita katika shule hiyo.Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
Wahitimu wa kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Wasichana ya Weruweru wakiimba wakati wakielekea ukumbini kwa ajili ya kuanza rasmi kwa sherehe ya kuwaaga.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru Rosemery Tarimo akimuongoza mgeni rasmi katika mahafali ya 31 ya kidato cha sita ,Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania ,Joel Raulant (kulia) wakati wakielekea ukumbini kwa ajili ya sherehe za mahafali hayo.
Mgeni rasmi katika mahafali ya 31 katika shule ya sekondari ya Wasichana ya Weruweru ,Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania,Joel Raulant akiingia ukumbini pamoja na Mkuu wa shule hiyo Rosemery Tarimo.
Mgeni rasmi ,Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania,Joel Raulant na wageni wengine wakiwa wamesimama wakifuatilia wimbo wa shule hiyo wakati ukiimbwa na wanafunzi katika mahafali hayo.
Wanafunzi wanaohitimu kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Wasichana ya Weruweru wakiimba wimbo wa shule.
Walimu na watumishi wengine wa shule hiyo wakifuatilia sherehe ya mahafali hayo.
Mkuu wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru,Rosemery Tarimo akitoa taarifa ya shule hiyo kwa mgeni rasmi wakati wa mahafali hayo ya 31 ambapo jumla ya wanafunzi 390 wamehitimu.
Wahitimu wakifuatilia taarifa ya shule hiyo iliyokuwa ikitolewa na Mkuu wa shule hiyo ,Rosemery Tarimo.
Wanafunzi wanaohitimu kidato cha sita katika shule hiyo wakisoma risala mbele ya mgeni rasmi.
Mzazi mualikwa ,Jaji Amir Mruma akizungumza kwa niaba ya wazazi wenye watoto wanaosoma katika shule hiyo.

No comments: