Monday, April 18, 2016

JAJI MKUU WA TANZANIA MHE. MOHAMED CHANDE OTHMAN AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA JAJI MKUU WA MAHAKAMA YA CHINA MHE. ZHANG JIANNAN LEO JIJINI DAR ES SALAAM

 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akiwa ameongozana na Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang Jiannan (kuahoto) mara baada ya kumpokea katika viwanja vya Mahakama ya Rufaa leo jijini Dar es salaam. Mhe. Zhang Jiannan pamoja na ujumbe wake yupo nchini kwa ziara ya kikazi kwenye Mahakama ya Tanzania kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa utendaji kazi na kuimarisha ushirikiano baina ya Mahakama ya Tanzania na China. 
 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akisalimiana na baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China mara baada ya kuwakaribisha   Mahakama ya Rufaa leo jijini Dar es salaam.
  Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (katikati) akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja kati ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China uliolenga kukuza ushirikiano na kubadilishana uzoefu wa utendaji wa Mahakama za Tanzania na China leo jijini Dar es salaam. 
 Baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa mkutano wa pamoja ulioongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania na Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China.
   Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na wale wa Mahakam Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China wakibadilisha uzoefu wa shughuli za kimahakama na masuala mbalimbali ya utendaji wakati wa mkutano wa pamoja ulioongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania na Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China jijini Dar es salaam.
 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo. Kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang Jiannan
 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akimweleza jambo Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang Jiannan wakati wa mkutano huo.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (kushoto) akieleza namna Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China inavyofanya kazi leo jijini Dar es salaam wakati wa kikao cha pamoja kilichowahusisha Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na China. Wengine  ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (katikati) na Jaji Kiongozi Mhe. Shaban Lila.  
 Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (kushoto) akipokea zawadi ya kinyago kutoka kwa Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman.
  Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman mbele ya Jengo la Mahakama ya Rufaa.
 Jaji Kiongozi wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Shaban Lila(kulia) akimweleza jambo jaji wa Mahakamu Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China mara baada ya kumkaribisha Ofisini kwake Mahakama Kuu leo jijini Dar es salaam.
Jaji Kiongozi wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Shaban Lila(kulia) akiwa katika mazungumzo na Jaji wa Mahakama Kuu ya China na baadhi ya Majaji kutoka  Mahakama hiyo waliomtembelea Ofisini kwake Mahakama Kuu jijini Dar es salaam.
 Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (wa pili kutoka kushoto mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman (katikati) na baadhi ya watendaji wa Mahakama ya Tanzania mbele ya Jengo la Mahakama ya Rufaa leo jijini Dar es salaam.
 Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang ( kushoto) akiagana na  Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman (kulia) mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo naye leo jijini Dar es salaam. Picha/Aron Msigwa.

No comments: