Monday, April 25, 2016

HOSPITALI YA TENGERU YAKABILIWA NA UHABA WA VITANDA

picha ikionyesha wafanyakazi wa NSSF pamoja na mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Tengeru katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi msaada wa vyandalua
wafanyakazi wa NSSF wakiwa wanabadilishana mawazo nje ya hospitali hiyo 
mmoja ya wagonjwa akiwa amekaa kitanda kimoja na watoto wawili wakiwa kila mmoja ana mama yake


Na Woinde Shizza,Arusha


Hospitali ya wilaya ya Tengeru (Patandi) inakabiliwa na ukosefu wa vitanda hali ambayo inapelekea wagonjwa kulala zaidi ya mmoja katika kitanda kimoja.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi hili wagonjwa hao mara baada ya kupokea msaada wa vyandalua kutoka kwa wafanyakazi wa mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF) tawi la Arusha walisema kuwa wao kama wagonjwa wa hospitali hiyo wamekuwa wanapata tabu sana haswa wakati wakiandikiwa kulazwa kwani wana banana sana na wakati mwingine wanakosa kabisa vitanda.

Mmoja wa wagonjwa hao ambaye alijitambulisha kwa jina la Anna Akyoo alisema kuwa wamekuwa wakilala wagonjwa wawili hadi watatu hali ambayo inawafanya wajisikie vibaya kwani wana banana sana katika vitanda hivyo vichache.

Unajua mfano mimi nimekuja hapa unaniona nipo na mtoto wangu lakini tunalala wawili kwaiyo ukichanganya na watoto wetu maana unaona hii ni wodi ya mama na mtoto tunakuwa wanne kweli tunaomba sana serekali ituangalie sana hospitali hii kwani tunateseka nasio kuteseka tu sasa tunavyobanana hivi muda mungine tunaweza ata kutoka na magonjwa mengine umu,unakutwa umemleta labda mtoto anaumwa ugonjwa huu tukija apa huku kubanana badala ya kupona anatoka na gonjwa lingine kweli watuangalie sana”alisema Lea Mmari' 

Kwa upande wake mganga mkuu wa hospitali hiyo ya wilaya ya Tengeru Ukio Kusirigwa alisema kuwa ni kweli tatizo la vitanda lipo lakini sio kubwa kikubwa kinachowakabili hospitali hiyo ni kukosekana kwa wodi za kuwalaza wagonjwa hali ambayo inawafanya wawabananishe katika vitanda hivyo.

“unajua siwezi sema kuwa tatizo la ukosefu wa vitanda hamna hapana lakini shida kubwa ata tukipata vitanda sasa ivi tutaviweka wapi na wodi zimeja ,hospitali hii ya wilaya imekuwa inapokea wagonjwa wengi kutoka tengeru hapa ,mererani na ata kia na kikatiti maana hii ndio hospitali kubwa ya wilaya iliopo karibu hivyo kwa wingi huo na ukiangalia wodi ni chache tunakosa jinsi hivyo inatubidi wagonjwa walale wawili wawili ili waweze kupata huduma”alisema Kusirigwa.

Aidha aliwaomba wadau pamoja na serekali kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kama vile wafanyakazi wa NSSF tawi la Arusha walivyojitokeza kuja kutoa misaada angalau ya vitanda,majengo na kikubwa zaidi aliwaomba sana waisaidie hospitali hiyo kujenga wodi kwa ajili ya wagonjwa wakiwemo wakina mama na mtoto.

Naye meneja wa NSSF Frank Maduga alisema kuwa wao kama wafanyakazi wameamua kujichanga na kuweza kusaidia hospitali hii kwa kuwapa vyandalua hii ikiwa ni kuunga mkono kampeni ya kupiga vita ugonjwa wa malaria.

Alisema kuwa mpaka sasa wameshatoa vyandarua 184 katika hospitali tofauti ikiwemo ya Mount meru ,St Elizabeth,Levolosi pamoja na kwenye vituo vya kulelea watoto yatima na wasiojiweza ambacho ni kituo cha walemavu Usa river na hawataishi hapo tu wao kama wafanyakazi wamejipanga kila mwisho wa mwezi kutoa msaada katika kila sehemu ambayo inamlenga mwananchi.

Alitoa kwa wadau mbalimbali kujitoa kwa kuchangia na kusaidia kwa kutoa misaada katika sehemu mbalimbali ikiwemo watoto yatima ,wasio jiweza na hata katika hospitali zetu ili kuweza kuwapa moyo wahusika na sio kusubiri tu serekali ifanye ,kwani kutoa ni moyo ivyo kila mtu anaeguswa ajitokeze kutoa ikiwemo kuchangia wodi za hospitali hiyo.

No comments: