Monday, March 21, 2016

WAZIRI NNAUYE AZUNGUMZA NA WAKONGWE WA WANAMZIKI DANSI JIJINI DAR LEO.

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amezungumza na wadau wa mziki wa Dansi leo jijini Dar es Salaam na kusikiliza changamoto mbalimbali za wadau hao wa muziki huo wa Dance.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akizungumza na wanamziki wa Dansi leo alipokutana nao katika ukumbi wa vijana Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Godfrey Mungereza akizungumza na wakongwe wa muziki wa Dansi leo katika ukumbi wa Vijana Kinondoni jijini Dar es Salaam.  Kulia ni Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.
 Mkurugenzi wa bendi ya Muziki wa Dance nchini African Starz (Twanga Pepeta), Asha Baraka akizungumza katika mkutano wa wanamziki wa Dansi  na Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye 
 Mwanamziki wa Mziki wa Dansi, Duncan Nnjirima akichangia maada katika mkutano huo na Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.
 Wakongwe wa mziki wa Dansi wakimsikiliza Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo,Nape Nnauye leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Al-Hassan Michuzi.










No comments: