Saturday, March 5, 2016

WAFANYAKAZI WA BENKI YA CRDB TAWI LA WATER FRONT WATOA MSAADA KATIKA TAASISI YA OCEAN ROAD LEO.

KUELEKEA siku ya wanawake duniani  wafanyakazi wa benki ya CRDB tawi la Water front jijini Dar es Salaam leo wametoa msaada wa vitu mbalimbali pamoja na fedha katika taasisi ya Saratani ya Ocean Road jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuwasaidia baadhi ya wagonjwa waliopo katika hospitali hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Water Front jijini Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufika katika Taasisi ya magonjwa ya Saratani ya Ocean Road  jijini Dar es Salaam leo kwaajili ya kutoa masaada wa vitu mbalimbali.
Baadhi ya vitu vilivyotolewa na wafanyazi wa Benki ya CRDB tawi la Water Front jijini Dar es Salaam. 
 Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Water Front jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Water Front jijini Dar es Salaam wakitoa vitu kwenye gari kwaajili ya kutoa msaada katika Taasisi ya magonjwa ya Saratani  Ocean Road jijini Dar es Salaam leo.
......................................
Hata hivyo wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Water Front jijini Dar es Salaam wametoa elimu kwa wafanyakazi na wanakikundi cha  'The Great Ten'wa Kampuni ya Busines Times jijini Dar es Salaam kuhusiana na kufungua Akaunti ya MALKIA katika benki hiyo kwa kusherekea siku ya wanawake duniani ambayo kilele cha maadhimisho ya siku hiyo ni Machi 8 kwa kila mwaka.
Meneja Biashara wa Benki ya CRDB tawi la Water Front jijini Dar es Salaam, Adam Akaro (kulia) akizungumza na wafanyakazi wa kampuni ya Business Times wanaounda kikundi cha 'The Great Ten', kuhusiana na huduma wanaozitoa benki hiyo kuelekea siku ya wanawake duniani ambayo kilele chake ni Machi 8 kwa kila mwaka.  
 Meneja Biashara wa Benki ya CRDB tawi la Water Front jijini Dar es Salaam, Adam Akaro (kulia) na Meneja wa huduma kwa mteja wa benki ya CRDB tawi la water Front jijini Dar es Salaam wakiwa katika kikao na wafanyakazi wa wafanyakazi wa kampuni ya Business Times wanaounda kikundi cha 'The Great Ten'.
Mwanachama wa kikundi cha 'The Great Ten', Sebastian Sungi akifafanua jambo katika kikao kilichofanyika katika ofisi za  kampuni ya Business Times wanaounda kikundi cha 'The Great Ten'. Meneja Biashara wa Benki ya CRDB tawi la Water Front jijini Dar es Salaam, Adam Akaro (kulia) na Meneja wa huduma kwa mteja wa benki ya CRDB tawi la water Front jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa kikundi cha 'The Great Ten', Grace Ndossa akichangia maada katika kikao kilichofanyika katika ofisi za kampuni ya Business Times na wanakikundi cha 'The Great Ten' walipokuwa wanazungumza na  Meneja wa huduma kwa mteja wa benki ya CRDB tawi la water Front jijini Dar es Salaam wakiwa katika kikao na wafanyakazi wa wafanyakazi wa kampuni ya Business Times wanaounda kikundi cha 'The Great Ten'.
Baadhi ya wafanyakazi wa wafanyakazi wa kampuni ya Business Times wanaounda kikundi cha 'The Great Ten'.wakimsikiliza 
 Meneja Biashara wa Benki ya CRDB tawi la Water Front jijini Dar es Salaam, Adam Akaro jijini Dar es Salaam leo.

No comments: