Saturday, March 5, 2016

Tutumie Utamaduni Wetu kujenga Nchi - Mh. Nape

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akipiga ngoma alipokuwa akiwasili katika ukumbi wa Golden Jubelee Towers alipokuja kushiriki katika uzinduzi wa Video mpya ya Mshairi Mrisho Mpoto inayoitwa Sizonje .Wengine Pichani ni Mrisho Mpoto,Dr Mwaka na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sanaa Bi leah Kihimbi.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye Nape Nnauye akizindua rasmi video ya Sizonje,Kushoto kwake ni Mrisho Mpoto.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akiinadi video ya Sizonje kwa wadau mbalimbali waliofika kushuhudia uzinduzi huo.Nape aisema video hiyo inawakilisha serikali ya awamu ya tano na utumbuaji wa majipu.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akimkabidhi cheti cha pongezi kwa Msichana Butogwa Charles Shija aliyeongoza kitaifa katika mtihani wa kidato cha nne.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akimkabidhi cheti cha pongezi kwa Congcong Wang aliyeshika nafasi ya pili kitaifa katika mtihani wakidato cha nne.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akimkabidhi cheti cha ushujaa kwa kijana Salmin Selemani ambae alifanya vibaya katika mtihani wa kidato cha nne lakini hakukata tamaa na kujitokeza hadharani ili asaidiwe,Waziri Nape amejitolea kumwendeleza kijana uyu. Picha na Daudi Manongi.

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye amewataka watanzania kutumia utamaduni wetu kujenga nchi yetu.

Waziri nape ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa video ya mshairi Mrisho Mpoto mbele ya wadau mbalimbali wa sanaa kutoka kila kona ya jiji la Dar es Salaam waliofurika kuangalia uzinduzi huo ulioendana sambamba na mada kubwa mbili za utamaduni na lugha na kauli mbiu ya Kufeli elimu sio mwisho wa maisha.

“Serikali ya awamu ya Tano imejipanga vyema katika kutumia utamaduni wa nchi yetu kushape vijana wetu wawe na morali,wajitambue ili wafike mbali,tutatumia utamaduni huu kujenga nchi yetu kikamilifu kwani ni silaha tosha kuvutia hata nchi nyingine.Maisha sio rahisi,ni kuvumilia,kutokata tamaa na kuweka malengo.Safari tumeianza na tutafika mbali”Alisema Nape.

Pia Waziri uyo aliwataka watanzania kumuunga mkono Mrisho mpoto na kutomkatisha tamaa kwani anamsaidia rais wa awamu ya Tano Mhe.John Pombe Magufuli katika kutumbua majipu.Mbali na hilo alimshauri Mrisho mpoto kwenda mikoani kwani hata uko kina Sizonje wapo wengi muwaonyeshe kwamba iko njia kwa watu waliokata tamaa.

Kwa upande wake Mrisho mpoto aliwasii watanzania kujenga taifa letu na pia tujenge Kiswahili na kukitumia kama ajira  kwani ni lugha ya sita kwa sasa duniani.

“Lazima tujue kwamba Kiswahili ni lugha ya kibiashara,tuangalie fursa zilizopo kupitia Kiswahili kujipatia ajira kwani nchi kama Namibia,Zimbabwe wamepokea Kiswahili na wanaitaji kufundishwa zaidi na kwa namna hii izi zote ni fursa kwani lugha imekuwa bidhaa sasa”Alisema Mpoto.

Wakichangia katika mjadala uliopewa jina “kufeli elimu sio kufeli maisha” Bw.Ruge Mutahaba alisema kufeli darasani kusikuzwe na kuwataka vijana kutengeneza maono mapema kwani yatakuwa ndio mwongozo wa maisha yao yote na yatawafanya vijana kutokata tama mapema.

“Vijana Mjifunze kuwasiliana,muwe wabunifu,mjifunze kuwa na utaratibu wa kujifunza kitu kipya kila siku,pia mtengeneze jamii ya watu ambao ni watatua matatizo na sio watumikaji tu kwani kwenye matatizo ndo kwenye fursa zote,msiiachie serikali pekee kushughulikia huduma za jamii bali tumieni mwanya huo kuanzisha za kwenu”Alisema Ruge.

Naye mwakilishi kutoka TBL Bw George Kavishe aliwataka vijana kujua mihimili yao pamoja na uwezo wao na kwa kufanya ivyo watakuwa wamejua wapi wanacho na nini kinafaa kufanya ili kuboresha maisha yao.

Mjadala huo pamoja na uzinduzi wa video ya sizonje uliambatana na waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na michezo Mhe.Nape kuwapa vyeti vya pongezi na ushujaa vilivyoandaliwa na Mrisho Mpoto wanafunzi waliofanya vizuri na wale waliofanya vibaya katika mtihani wa kidato cha nne.

No comments: