Thursday, March 10, 2016

SPIKA JOB NDUGAI AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA JAMHURI YA KISOSHALISTI YA VIETNAM LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang leo mara walipokutana kwa ajili ya mazungumzo katika Hoteli ya Kilimanjaro 10 Machi, Jijini Dar es Salaam.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai pamoja na Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang wakiwa katika mazungumzo yaliyohusishwa na baadhi ya ujumbe toka nchi ya Vietnam na Tanzania leo mara walipokutana kwa ajili ya mazungumzo katika Hoteli ya Kilimanjaro 10 Machi, Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang (wa pili kushoto) akiongea na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (hayupo pichani) mara walipokutana kwa ajili ya mazungumzo katika Hoteli ya Kilimanjaro 10 Machi, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akiongea na baadhi ya vyombo vya habari mara baada ya mkutano uliofanyika kati ya Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai katika Hoteli ya Kilimanjaro 10 Machi, Jijini Dar es Salaam.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akiongea na baadhi ya vyombo vya habari mara baada ya kukutana na Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang katika Hoteli ya Kilimanjaro 10 Machi, Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Spika wa Bunge hilo, Mhe. Dkt. Tulia Ackson.
Baadhi ya ujumbe alifuatana nao Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang wakifuatilia mazungumzo yao leo mara walipokutana kwa ajili ya mazungumzo katika Hoteli ya Kilimanjaro 10 Machi, Jijini Dar es Salaam. PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO

No comments: