Friday, March 4, 2016

Serikali yamkabidhi Cheka Cheti cha pongezi kutokana na ushindi wake

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye(kulia) akiwa ameambatana na Bondia Francis Cheka (wapili kulia) alipotembelea Wizarani leo jijini Dar es Salaam na Serikali imemkabidhi Cheti cha pongezi. Kushoto ni Rais wa Chama cha ngumi Tanzania (TPBO) Yassin Adballah (Ustadh).
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye(katikati) akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa zoezi la kumkabidhi Cheti cha pongezi kutokana na ushindi Bondia Francis Cheka (kushoto) leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Makoye Alex Nkenyenge.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Makoye Alex Nkenyenge (aliyesimama) akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa zoezi la kumkabidhi Cheti cha pongezi Bondia Francis Cheka (wa pili kushoto) kutokana na ushindi wake leo jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye na wa mwisho kushoto ni Rais wa Chama cha Mchezo wa Ngumi Tanzania (TPBO) Yassin Adballah (Ustadh).
Bondia Francis Cheka akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa zoezi la kupokea Cheti cha pongezi kutoka kwa Serikali leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye,Rais wa Chama cha ngumi Tanzania (TPBO) Yassin Adballah (Ustadh) na Meneja wa Bondia huyo Chifu Ndambile Juma Ntinginya.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (wapili kushoto) akimsikiliza kwa makini Katibu Mtendaji wa BMT Mohamed Kiganja (aliyesimama) akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa zoezi la kumkabidhi Cheti cha pongezi Bondia Francis Cheka (kushoto) kutokana na ushindi wa Mkanda wa Uzito wa Super Middle wa Mabara wa WBF leo jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Makoye Alex Nkenyenge.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kulia) akimkabidhi Cheti cha pongezi Bondia Francis Cheka kutokana na ushindi alioupata katika pambano baina yake na Bondia Mserbia anayeishi Uingereza Geard Ajetovic (hayupo pichani) leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kulia) na Bondi Francis Cheka wakiwaonyesha waandishi wa Habari Mkanda wa uzito wa Super Middle wa Mabara ambao Cheka ameunyakuwa baada ya kushinda pambano la tarehe 27 Februari baina yake na Bondia Mserbia anayeishi Uingereza Geard Ajetovic (hayupo pichani) leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Meneja wa Bondia huyo Chifu Ndambile Juma Ntinginya. Picha na Frank Shija, WHUSM.

No comments: