Thursday, February 18, 2016

UZINDUZI WA MRADI WA AFYA BORA YA MAMA NA MTOTO ZANZIBAR.

 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Halima Maulid Salum akifungua warsha ya uzinduzi wa Mradi wa Afya bora ya mama na mtoto katika Hoteli ya Mzson Shangani Mjini Zanzibar.
 Mkurugenzi Idara ya Kinga na elimu ya afya Dkt. Mohd Dahoma akizungumza na washiriki waliohudhuria katika warsha ya uzinduzi wa mradi wa Afya bora ya Mama na Mtoto katika ukumbi wa Hoteli ya mazson Shangani mjini Zanzibar.
 Meneja wa Mradi wa Afya bora ya mama na mtoto kutoka Shirika la kuhudumia watoto Tanzania Dkt. Bernard Mbwele akitoa maelezo juu ya mtazamo wa mradi huo kwa washiriki katika Hoteli ya Mazson Mjini Zanzibar.
  Meneja Msaidizi wa Shirika la kuhudumia watoto Dkt. Awrad Saleh akiwasilisha mada ya majukumu ya waangalizi na wakaguzi wa Mradi wa Afya bora ya mama na mtoto wakati wa uzinduzi wake.
  Daktari dhamana Kanda ya Unguja Dkt. Fadhil Mohd akitoa mchango wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Afya bora ya mama na mtoto katika Hoteli ya Mzson Shangani Mjini Zanzibar.
 Baadhi ya washiriki katika uzinduzi wa Mradi wa Afya ya mama na mtoto uliofanyika Hoteli ya Mzson Shangani wakifuatilia uzinduzi huo.
PICHA NA ABDALLA OMARA/MAELEZO ZANZIBAR.

No comments: