Saturday, February 20, 2016

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

 Serikali yaiomba jamii ya kimasai kuendelea kudumisha amani na utulivu ulipo nchini; https://youtu.be/mdBojN2LoWk  

Spika wa bunge Job Ndugai amesema Tanzania na nchi ya Sweden zitaendelea kushirikiana katika nyaja mbali mbali ili kuleta maendeleo; https://youtu.be/lJqfHv3j9M8  

Wanafunzi 16 wa chuo kikuu cha Mtakatifu Joseph kilichopo mkoani Ruvuma wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kufanya fujo;https://youtu.be/NTRkhZ4kC28  

Serikali ya Tanzania na Rwanda zimekubaliana kushirikiana katika kutatua mgogoro wa kisiasa katika nchi ya Burundi;https://youtu.be/uc0uiTAAKbI  

Sensa ya kilimo, uvuvi na ufugaji nchini inatarajiwa kuanza Februari 23 mwaka huu; https://youtu.be/8UufjeT2o5w   

Benki M yaanzisha huduma ya mpya ya Money moja kwa moja kuwarahisishia wateja wake pindi watakapohitaji kutoa pesa katika akaunti zao; https://youtu.be/U4qx4EFmsXY  

Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Mhe Nape Nnauye amsimamsisha kazi katibu mtendaji wa baraza la michezo Tanzania kwa kutoridhishwa na utendaji kazi wake;https://youtu.be/BIlxnR9npOE  

Tiketi kwa ajili ya mchezo  wa watani wa jadi baina ya Simba SC na Yanga zaanza kuuzwa hii leo; https://youtu.be/Ae_KWLGrKJg  

Shirikisho la vyuo vya elimu ya juu CCM visiwani Zanzibar limeitaka tume ya uchaguzi ZEC kuwa makini na uwepo wa makamishina wa chama cha wananchi CUF katika vikao vya tume ya uchaguzi Zanzibar; https://youtu.be/BUyqUC93RtI  

Mkuu wa mkoa wa Kaskazin Pemba,Mhe.Omary Khamis Othman achukuizwa na kitendo cha watendaji wa wizara ya kilimo visiwani humo kuuza mashamba ya serikali; https://youtu.be/ODaORN-b2Xw

Wananchi mkoani Tabora wametakiwa kufuata sheria na taratibu wakati wa ununuzi wa maeneo ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima; https://youtu.be/xevgvUP4f68

Wafanyakazi wa taasisi ya uhasibu nchini TIA wametakiwa kufanya kazi kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa;https://youtu.be/n1gCzlJKLgs  

Tume ya vyuo vikuu nchini TCU yafuta  kibali cha usajili wa vyuo vikuu vishiriki viwili; https://youtu.be/93fRBknYuRQ

Mwanamke mmoja huko mkoani Geita achinjwa na kufariki dunia huku mumewe akijeruhiwa kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kukopa fedha. https://youtu.be/nKX0-ZRLB2A  

Tume ya vyuo vikuu nchini TCU, yavifutilia mbali vyuo vikuu vitatu nchini kwa kushindwa kusimamia ubora, na taaluma pia kukiuka sheria ya uendeshaji wa vyuo. https://youtu.be/kOOP7D00Yag  

Serikali yaingilia kati mgogoro mkubwa ulioibuka baina ya wafugaji wa jamii ya kimasai na wale wa kibarbaig waliokuwa wakituhumiana kuibiana ngombe na kuupatia utatuzi.https://youtu.be/OEArqoc1WAA  

Waziri mkuu Mhe.Kassim Majaliwa afanya ziara ya kushitukiza katika bandari ya Tanga na kumuagiza meneja wa banadari hiyo kuandika barua ya kujieleza kufuatia ukiukwaji wa taratibu za manunuzi. https://youtu.be/y5UxC7uyyNc  

Wachimbaji wa madini ya dhahabu mkoani Shinyanga huenda wakaanza kuzalisha kwa tija baada ya kutengenezewa mashine itakayo rahisisha kuvuta udongo wenye madini kutoka ardhini.https://youtu.be/U9ZCiV4_cqs  

Siku chache baada ya naibu waziri Suleiman Jaffo kuipa maagizo hospitali ya Zakheim, wananchi wakiri kuwepo kwa mabadiliko makubwa ukilinganisha na hapo awali. https://youtu.be/6VG3NaEA-14  

Baadhi ya wanafunzi, wazazi na walimu watoa mtazamo tofauti juu ya matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa hapo jana.https://youtu.be/ENEaqif5rRs

No comments: