Monday, February 1, 2016

JOVAGO TZ YAWATAKA WATANZANIA KUTUMIA INSTAGRAM KUTANGAZA UTALII.

Meneja wa mawasiliano wa Jovago,Liliani Kisasa akizungumza na waandishi wa habari juu ya kutumia mitandao ya kijamii kwa maendleo ya Taifa katika mkutano uliofanyika kinondoni jijini Dar es Salaam.


TAASISI ya kufanya Biashara mitandaoni ya Jovago Tanzania imewataka watanzania kutumia fursa ya matumizi ya mitandao ya kijamii kuitangaza nchi katika sekta ya utalii kimataifa.

Wito huo imetolewa na Mkurugenzi wa Jovago Afrika Mashariki Estelle Verdier –Watine alipokuwa akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya umuhimu wa matumizi ya mtandao wa Instagram kutangaza utalii wa Tanzania.

“Tanzania ni nchi inayoongoza kwa matumizi ya instagram Africa hivyo fursa hiyo ni vyema ikatumika vyema katika kupandisha utalii wa taifa hili kuliko kupost vitu ambavyo avina faida kwa taifa” alisema Estelle.

Alisema kuwa kwa kuthamini hilo tasisi ya Jovago Tanzania imeandaa shindano la kuweka pichakatika Insrgram hivyo atakaye pata like nyingi ataweza kupata ofa ya kulala katika Hotel ya Ramada iliyopo Mbezi Beacha Dar es Salaam.

Kwa upande wake afisa habari wa kampuni hiyo Liliani Kisasa aliwatka watanzania kuchangamkia fursa hiyo hili waweze kufurahia siku hiyo wakiw ana wenzi wao.

Alisema ni jambo zuri sana kama mmoja ya watu kutoka hapa nchini.
Liliani Kisasa PR manager Jovago.
Liliani Kisasa PR manager Jovago.
Estelle Verdier -Watine East Africa Manger Jovago .Com akizungumza na wana habari.
Liliani Kisasa PR manager Jovago akiojiwa na ITV.

No comments: