Friday, January 22, 2016

JK atunukiwa Shahada ya heshima ya Mahusiano ya Kimataifa OUT

Na Raymond Mushumbusi Maelezo

Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ametunukiwa Shahada ya heshima ya udaktari wa falsafa wa mahusiano ya kimataifa Leo Jijini Dar es Salaam katika mahafaliya 30 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania.

Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amesema amefarijika sana kutunukiwa shahada hiyo ya heshima itolewayo na Chuo kikuu Huria Tanzania kwa watu ambao wametoa mchango katika maendeleo katika jamii kupitia nafasi zao kiutendaji.

“Naipokea heshima hii toka Chuo Kikuu Huria Tanzania kwa moyo mmoja kwani wameona mchango ambao nimeutoa nilipokuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Awamu ya Nne hivyo basi nitaendeleza mahusiano na ushirikiano kimataifa”.Alisema Mhe. Dkt Kikwete.

Mbali na Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kuna baadhi ya maraisi na wakuu mbalimbali duniani waliwahi kupata Shahada za heshima toka Chuo Kikuu Huria Tanzania ambao ni Rais wa Awamu ya kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais wa Awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Rais wa Awamu ya tatu Benjamin William Mkapa, Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini Hayati Nelson Mandela na Dkt Koichiro Mastuura Mkurugenz iwa UNESCO.

Chuo kikuu Huria cha Tanzania kimetoa jumla ya wahitimu 69 wawili Shahada maalum na 67 ni Shahada, Stahahada na Astashahada, ambapo Shahada ya uzamivu ni wahitimu watatu, Shahada ya uzamili ni wahitimu 20, Shahada wahitimu 22,Stashahada wahitimu 15 na Astashahada wahitimu 6.

Tangu kuanzishwa kwa Chuo Kikuu Huria Tanzania mwaka 1992 jumla ya wahitimu 25,908 wametunukiwa Shahada mbalimbali na haya ni mahafali ya 30 tangu chuo kuanzishwa.
Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ( Kulia) akifatilia kitabu cha mahafali ya 30 ya Chuo kikuu Huria Tanzania yaliyofanyika Jijini leo Dar es Salaam. kushoto ni Prof Suh Chae-Hong Rais wa Chuo cha Chosun kilichopo Korea ya Kusini..
Maandamano ya wanataaluma katika Mahafali ya 30 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Dkt Asha Rose Migiro akifungua rasmi mahafali ya 30 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Dkt Asha Rose Migiro akimtunuku Shahada ya ya heshima ya udaktari wa falsafa ya mahusiano ya kimataifa Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete katika maafali ya 30 ya Chuo kikuu Huria Tanzania yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Dkt Asha Rose Migiro akimpongeza Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kumtunuku Shahada ya heshima ya udaktari wa falsafa ya mahusiano ya kimataifa katika mahafali ya 30 ya Chuo kikuu Huria Tanzania yaliyofanyika leo Jijini Dare s Salaam.
Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wanataaluma na wageni katika maafali ya 30 ya Chuo kikuu Huria Tanzania yaliyofanyika leo Jijini Dare s Salaam.
Baadhi ya wahitimu wa shahada mbalimbali kutoka Chuo kikuu Huria Tanzania.

No comments: