Saturday, January 30, 2016

FLAVIANA MATATA NA MO DEWJI FOUNDATION WAKABIDHI MSAADA WA CHOO SHULE YA MSINGI MSINUNE, BAGAMOYO

002Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Francesca Tettamanzi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msinune iliyopo Bagamoyo, Pwani. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msinune iliyopo Bagamoyo, Msami Mgoto (kulia). Katikati ni Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation.
005Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation akisaini kitabu cha wageni kwenye ofisi ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msinune iliyopo Bagamoyo, Msami Mgoto (kulia) alipowasili kwenye hafla fupi ya kukabidhi choo kilichojengwa kwa ufadhili wa Mo Dewji Foundation.
006Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation, Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Francesca Tettamanzi wakiwa pamoja na baadhi ya watu walioongozana nao wakielekea kwenye eneo la tukio.
008
Muonekano wa jengo la choo ambalo limejengwa kwa ufadhili wa Mo Dewji Foundation.
012
Muonekano wa choo ambacho kilikuwa kikitumika awali kabla ya ujenzi wa choo kipya ambacho kimejengwa kwa ufadhili wa Mo Dewji Foundation.
010
Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation, Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Francesca Tettamanzi wakitoka kukagua vyoo hivyo kabla ya uzinduzi rasmi.
009
Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation katika tabasamu bashasha baada ya kukagua vyoo ambavyo vimejengwa kwa ufadhili wa Mo Dewji Foundation. 014
Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation (kushoto) na Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Francesca Tettamanzi kwa pamoja wakifunua kitamba kuzindua jiwe la msingi wakati wa hafla ya uzinduzi wa vyoo vya kisasa katika Shule ya Msingi Msinune iliyopo Bagamoyo, Pwani.
015
Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation (kushoto) na Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Francesca Tettamanzi wakionekana wenye nyuso za furaha baada ya kufunua kitambaa kwenye jiwe la msingi.
017019
Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Francesca Tettamanzi akikata utepe kuzindua rasmi choo cha kisasa katika shule ya Msingi Msinune kilichojengwa na Mo Dewji Foundation. Kushoto ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msinune iliyopo Bagamoyo, Msami Mgoto pamoja na wanafunzi wa shule hiyo wakishuhudia tukio hilo.
020025Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msinune, Msami Mgoto akitoa neno la shukrani kwa Mo Dewji Foundation na Flaviana Matata Foundation kwa msaada wa kuwajengea choo shuleni hapo.
026
Picha ya pamoja baada ya uzinduzi.
Taasisi ya Mo Dewji ikishirikiana na Taasisi ya Flaviana Matata, imekabidhi choo katika Shule ya Msingi Msinune ya Wilaya ya Bagamoyo, Mkoani Pwani kitakachosaidia wanafunzi wa shule hiyo.
Tukio la kukabidhi choo hicho limefanyika katika shule hiyo mapema leo na Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Taasisi ya Flaviana Matata, Bi. Flaviana Matata ambapo ameelezea kuwa, wamekua wakiwapatia wanafunzi wa Msinune vifaa vya shuleni tangu mwaka 2014 na mwanzoni mwa mwaka jana aliombwa kuwa mlezi wa Shule na kuweza kusaidia kutatua changamoto zinazoikabili shule hiyo ikiwemo suala hilo la vyoo vya waalimu na wanafunzi, madarasa pamoja na nyumba za walimu.
Flaviana amesema baada ya kuguswa aliweza kumshirikisha Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Mohammed Enterprises (MeTL Group), Mohammed Dewji, alikubali kutoa msaada huo kupitia taasisi yake hiyo ya Mo Dewji Foundation na kuweza kujenga choo hicho chenye matundu nane.
Kwa upande wake, Mkuu wa Shule hiyo ya Msinune, Bw. Msami Mgoto ameshukuru taasisi ya Mo Dewji kwa msaada wa kufadhili ujenzi wa choo hicho huku akielezea kuwa itasaidia wanafunzi zaidi ya 300 wanaosoma hapo licha ya kuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya majengo.
Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Msinune, Ramadhani Mtokeni aliishukuru Taasisi ya Mo Dewji kwa niaba ya wananchi wa kijiji cha Msinune huku akiomba iendelea kuwasaidia pindi wanapokuwa na matatizo.
Kwa upande wa mwakilishi kutoka Mo Dewji Foundation, Francesca Tettamanzi amepongeza juhudi za Flaviana Matata za kusaidia jamii ikiwemo kukua kwa elimu hapa nchini hivyo wataendelea kushirikiana naye bega kwa bega.
Francesca ameongeza kuwa, Mo Dewji kupitia msaada huo, wanafunzi watakuwa katika mazingira mazuri na safi kwa afya zao ikiwemo kusoma bila kuwa na tatizo la awali la choo, kwa sasa na miaka ijayo choo hicho kitakuwa mkombozi na msaada mkubwa.

No comments: