Sunday, December 20, 2015

KAMPUNI YA ULINZI YA SGA YATOA MSAADA WA MASHINE YA KUPUMULIA NA MASHUKA WODI YA WATOTO MWANANYAMALA

Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ulinzi ya Security Group Africa (SGA), Eric Sambu (kulia) akimkabidhi mshine ya kupumulia na mashuka, Mratibu wa Tiba katika Hospitali ya Mwananyamala, Dk Daniel Nkungu. Makabidhiano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki. Katikati yao ni Meneja Mahusiano kwa wateja wa SGA, Sophia Luhikula.
 Vitu vilivyotolewa msaada Hosipitalini hapo.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ulinzi ya Security Group Africa (SGA), Eric Sambu (kulia) akimkabidhi mshine ya kupumulia na mashuka, Mratibu wa Tiba katika Hospitali ya Mwananyamala, Dk Daniel Nkungu. Makabidhiano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Mahusiano kwa wateja wa SGA, Sophia Luhikula.
 Baadhi ya watumishi wa kitengo cha Ambulance cha SGA 
 Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ulinzi ya Security Group Africa (SGA), Eric Sambu akizungumza wakati wa kutoa msaada huo.
 Wafanyakazi wa SGA wakibeba msaada huo.
Habari na picha: Father Kidevu Blog

KAMPUNI ya Ulinzi ya Security Group (T) imetoa msaada wa mashine moja ya kupumlia na mashuka 40 kwa wodi ya watoto katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam

Kampuni ya SGA ilikabidhi mashine hiyo ya kupumulia na mashuka vyote vikiwa na thamani ya Sh milioni tano kwa wodi ya watoto Hospitali ya hapo na kusema hiyo ni kuonyesha jinsi gani wana jali afya za watanzania ambao wanafanyakazi nao.

“Nifuraha yetu kuona familia zetu zipo katika afya njema, lakini pia ulinzi wa mali zetu unaenda vizuri, hivyo leo tumeona tujitoe kidogo kukumbuka jamii yetu hasa watoto ambao ndio taifa la kesho,” alisema Mkurugenzi Mkuu wa SGA, Eric Sambu.

Sambu alisema huo ni muendelezo wa kurejesha kile wanachopata kwa jamii ili kujenga mahusiano mazuri na wataendelea kufanya hivyo kila inapo wezekana.

Akipokea msaada huo, Mratibu wa tiba hospitalini hapo, Dk Daniel Nkungu wanaishukuru kampuni hiyo kuwakumbuka na kuweza kuwasaidia msaada huo ambao kwa kiasi kikubwa utasaidia ufanisi katika utendaji kazi wao na kupunguza vifo vya watoto wachanga.
Picha ya pamoja ilipigwa 
 Wafanyakazi wakiwa wameshika mashuka waliyokabidhi.
 Wafanyakazi wa SGA wakirejesha mashuka hayo katika boxi.
 Baada ya hapo wafanyakazi walishiriki katika tafrija fupi ya kufunga mwaka na kusherehekea mwaka 31 tangu kuanzishwa kwa kampuni hiyo nchini ambapo awali ilijulikana kama Group 4. 
 Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ulinzi ya Security Group Africa (SGA), Eric Sambu akizungumza na wafanyakazi wakati wa tafrija.
 Wafanyakazi wakimsikiliza...
 Waliwasikiliza viongozi wao mbalimbali.
 Wakuu mbalimbali wa vitengo walizungumza...
 wafanyakazi walijumuika pamoja na kufurahi.
 Chakula kizuri kiliandaliwa na watu walikula vya kutosha na kupata vinywaji vya kila namna
Watu walikula chakula na kufurahi,

No comments: