Thursday, December 17, 2015

BANKI YA BARCLAYS WAZINDUA OFISI MPYA JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

Mwenyekiti wa bodi wa Benki ya Barclays hapa nchini, Ramadhani Dau akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ofisi mpya kwenye ghorofa ya pili ya jengo la benki hiyo lililopo jengo la Makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Mkurugenzi mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Tanzania, Kihara Maina akiwa na baadhi ya wadau wa benki hiyo wakati wa kuzindua ofisi ya benki hiyo ghorofa ya pili ya benki hiyo.
Mwenyekiti wa bodi wa Benki ya Barclays hapa nchini, Ramadhani Dau  akifungua kitambaa kuashiria uzinduzi wa ofisi ya benki hiyo  katika jengo la benki ya Barclays ghorofa ya pili leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Tanzania, Kihara Maina akishuhudia wakati akifungua kitambaa hicho.
Mkurugenzi mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Tanzania, Kihara Maina akizungumza na wafanyakazi wa benki ya Barclays hapa nchini (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Barclays hapa nchini wakimsikiliza Mkurugenzi mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Tanzania, Kihara Maina.

Baadhi ya wanabodi ya benki ya Barclays wakimsikiliza Mkurugenzi mkuu mtendaji wa benki ya Barclays Tanzania, Kihara Maina mara baada ya kuzindua ofisi mpya leo jijini Dar es Salaam. 

No comments: