Friday, November 27, 2015

HABARI KUTOKA VITUO VYA TELEVISHENI


Hatimaye maafisa ardhi 10 waliotupwa rumande na mkuu wa wilaya ya Kinondoni baada ya kuchelewa kazini,waanza rasmi kazi yao leo. https://youtu.be/7TM2U2RM1fE

Makamo wa Rais Bi.Samia Suluhu awataka wanawake nchini kushirikiana katika masuala ya kuwaletea maendeleo badala ya kuendekeza tabia isiyofaa ya kubezana. https://youtu.be/sRA9B8U6z9I

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam amepiga marufuku biashara holela za vyakula, matunda , pombe za kienyeji, maji ya viroba pamoja na juice lengo likiwa ni kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu. https://youtu.be/jTQzo3-x_q4

Rais John Mafuguli atembelea ofisi ya waziri mkuu na kufanya mazungumzo na Mh.Kassim Mjaliwa kwa muda wa saa 1. https://youtu.be/vn1Z21dos8M

Wachimbaji wadogo wa dhahabu waliofunikiwa na kifusi siku chache zilizopita wapatiwa matibabu na mganga wa jadi baada ya kushindwa kumudu gharama za matibabu hospitali ya Muhimbili. https://youtu.be/L1mTzX0lul4

Baadhi ya vijiji vilivyoko katika manispaa ya Iringa vyaiomba serikali kwa kushirikiana na wadau wa masuala ya afya kushughulikia kero ya uhaba wa vyumba vya wagonjwa. https://youtu.be/a1Kvl3bY2Hs

Balozi wa Ufaransa nchini Malika Berak atembelea makao makuu ya kampuni ya SUPERDOLL na kusifu uhifadhi wa matairi unaofanywa na kampuni hiyo. https://youtu.be/F4jq4WPd0iU

Mahakama kuu kanda ya Mwanza yafuta zuio la Polisi juu ya kuagwa kwa mwili wa aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema mkoni Geita. https://youtu.be/VyRSi6J7oh0

Imeelezwa kuwa kumekuwepo ongezeko kubwa la wabunge vijana katika bunge la 11 huku pia kukiwepo ongezeko kubwa la watoto wa viongozi. https://youtu.be/jwcyS42ePCc

Jiji la Arusha liko kwenye mpango maalum wa uboreshaji wa mipango miji utakaoboresha muonekano wa jiji na kuwa na hadhi inayostahili. https://youtu.be/hv-qfDl0mAI

Baadhi ya wananchi wa jimbo la Tabora mjini wafungua kesi katika mahakama kuu kanda ya Tabora kupinga matokeo ya ubunge wa jimbo hilo. https://youtu.be/fthVPDd3LBc

Katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue, apiga marufuku utengenezaji na uchapishaji wa kadi za Christimas na mwaka mpya kwa gharama za serikali kwa mwaka huu. https://youtu.be/Ia7hVfktHqY
Wananchi wilayani Ulanga waiomba serikali kuingilia kati mgogoro uliopo kati ya wakazi hao na halmashauri ya wilaya hiyo. https://youtu.be/-B_XZMN_1d8

Mahakama kuu kanda ya Mwanza yafutilia mbali zuio lililowekwa na jeshi la polisi la kuzuia kuugwa mwili wa marehemu Alphonce Mawazo; https://youtu.be/sR13mGsq5f0

Jeshi la polisi mkoani Kigoma limethibitisha kuwafukuza kazi askari polisi watatu kwa tuhuma za kusambaza taarifa za uongo; https://youtu.be/DaNThhodz08

Mkuu wa wilaya ya Korogwe mkoani Tanga ameagiza kukamatwa kwa mratibu wa maabara wa halimashauri hiyo kwa tuhuma za wizi wa vifaa vya maabara; https://youtu.be/p8_RVbDv20Q

Fahamu zaidi kuhusu watu sita walioishi chini ya ardhi kwa muda wa siku 41 wilayani Kahama mkoani Shinyanga;https://youtu.be/HCmUO17xMm0

Serikali ya Tanzania imeshauriwa kuiboresha sekta ya utalii nchini ili kukuza idadi ya watalii wanaokuja nchini ili kusaidia kukuza pato la taifa; https://youtu.be/yETj6TSJbjI

Serikali imetoa mda wa siku saba kwa wafanyabiashara waliokuwa wapangaji wa soko la Mwanjerwa jijini Mbeya kuomba upya nafasi za kufanya biashara katika soko hilo; https://youtu.be/Gz6IQUpq3dc

Mashindano ya kimataifa ya mbizo za magari, zamani yakijulikana kama East African Safari Classic Rally yamezinduliwa jijini Arusha; https://youtu.be/tEsqH8vKR20

Kocha mkuu wa klabu ya Arsenal mzee Arsene Wenger, amesema ataingia sokoni wakati wa dirisha dogo la usajili kuhimarisha kikosi chake; https://youtu.be/945BEZ9OpDk

No comments: