Friday, October 23, 2015

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO,AMOS MAKALLA ASHIRIKI KIFUNGUA KINYWA NA WAFANYAKAZI NA WATEJA WA BENKI YA NMB TAWI LA NELSON MANDELA-MOSHI

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Amosi  Makalla leo asubuhi ameshiriki chai na wafanyakazi na wateja waNMB Tawi la Moshi na kuipongeza benki ya NMB kwa kuwa benki 10 bora Afrika mashariki, benki inayoongoza kwa kuwa na matawi mengi nchini, benki inayoongoza kwa kutengeneza faida na kusaidia jamii, benki ya riba na gharama nafuu nchini na benki yenye  huduma bora kwa wateja nchini.


Pamoja na mafanikio hayo ameishauri benki hiyo kuendelea kuwa wabunifu wa bidhaa na kuendeleza huduma bora hasa katika kipindi hiki cha ushindani.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Amosi  Makalla kushoto akipata chai asubuhi leo chai iliyoandaliwa na benki ya NMB tawi la Nelson Mandela Moshi,kulia 
Meneja wa Tawi hilo 
Emanuel  Kishosha.
 Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Amosi  Makalla  akizungumza na wafanyakazi na wateja wa benki ya NMB tawi la Nelson Mandela Moshi leo mara bada ya kushiriki pamoja na wafanyakazi pamoja na wateja wa benki hiyo leo katika tawi la Nelson Mandela Moshi.
 Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Amosi  Makalla akilishwa keki na mfanyakazi wa benki ya NMB tawi la Nelson Mandela Moshi leo aliposhiriki pamoja katika kifungua kinywa.

 Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Amosi  Makalla akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi pamoja na wateja wa benki hiyo katika tawi l Nelson Mandela.

No comments: