Thursday, October 22, 2015

Magufuli afanya mikutano ya kampeni katika jimbo la Kibamba,Kawe,Chalinze,Kibaha vijijini na Kibaha mjini jijini Dar leo.

Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akimnadi Mgombea Ubunge wa jimbo la Chalinze,Ndugu Ridhiwani Kikwete.Dkt Magufuli amefanya mikutano ya kampeni katika jimbo la Kawe,Chalinze,Kibaha vijijini,Kibamba na Kibaha mjini.
PICHA NA MICHUZI JR-DAR ES SALLAAAM
Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akimkabidhi kitabu cha Ilani ya ccm kwa Mgombea Ubunge wa jimbo la Kibaha vijini .Nduggu Hamoud Abuu Jumaa.
 Umati wa wakazi wa jimbo la Kawe wakifuatilia mkutano wa kameni
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa-CCM,Dkt Gharib Bilal akimuombea kura za ushindi Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika viwanja vya Bunju jioni ya leo jijini Dar.
 Sehemu ya umati wa watu wakiwa wamekusanyika viwanja vya Bunju,kwenye mkutano wa kampeni jimbo la kawe jioni ya leo ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alijinadi na kuomba kura za ushindi ifikapo Oktoba 25 kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.
 Sehemu ya umati wa wakazi wa jimbo la kawe wakishangilia kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Bunju jioni ya leo jijini Dar
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Mungano kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Kawe,Keppy Warioba viwanja vya Bunju jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni.
Wananchi wa jimbo la Kawe wakishangilia jambo wakati Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Bunju,jijini Dar
Wanachama wa CCM wakishangilia kwa staili ya namna yake,kwenye mkutano wakampeni mjini Kibaha.
Mgombea Ubunge wa jimbo la Kibaha mjini Ndugu Silvestry Koka akijinadi mbele ya wakazi wa mji wa kibaha kwenye mkutano wa kampeni,ambapo pia Mgombea Urais wa CC Dkt Magufuli alijinadi na kuomba kura.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Mungano kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Kawe,akijinadi viwanja vya Bunju jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni.
Mmoja wa wafuasi wa CHADEMA alipojichanganya kwenye mkutano wa CCM,maara baada ya kuutiwa na sera za Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alipokuwa akijinadi mbele yao wananchi
Siasa sio uhasama
 Wananchi wakifuatilia mkutano wa kampeni wa Dkt John Pombe Magufuli
 Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli akijinadi kwa wakazi wa Tegeta jioni ya leo alipokuwa akielekea mjini Chalinze kuwahutubia wananchi kwenye mkutano wa kampeni
 Staili mpya ya Kumpokea Mgeni,Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alipokuwa akiwasili viwanja vya bunju,jimbo la Kawe kuwahutubia katika mkutano wa kampeni
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akibadilishana jambo na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa-CCM,Dkt Gharib Bilal
 Mjumbe wa Halmashauri kuu Taifa-CCM Mama Sophia Simba akimwombea kura Dkt Magufuli ili apate ridhaa ya wananchi na kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania,kwa kupata kura nyingi zinazotarajiwa kupigwa oktoba 25

No comments: