Friday, September 18, 2015

WANAWAKE:JIVUNIE KURA YAKO NDANI YA JAMII,EPUKA MCHEPUKO.

 HII NAFASI YA PEKEE NA ELEWA MAANA YA MABADILIKO WITO KWA WANAWAKE WOTE [WOMEN AS WINNERBREAD] ELISERENA KIMOLO MWENYEKITI UWT DMV NCHINI MAREKANI. 1.WITO KWA WANAWAKE WOTE.

Tumepata nafasi ya pekee mwanamke kuwa Makamu wa Rais,Mama Samia anafahamu fika matatizo ya mwanamke ndani ya familia,hivyo kwa mara ya kwanza huu ni ukombozi kwa mwanamket .

Tumepata mtetezi katika ngazi ya juu kwa sababu siku zote mwanamke ndie anayehusika zaidi na mambo ya familia , huku Nchini Marekani na nchi nyingine kama China au nchi zilizoendelea, Mwanamke anajulikana kama" WOMEN AS WINNERBREAD".Kwanini tunaitwa hivyo , Kwasababu ya jitihada zetu katika jamii.

Jitihada zetu za kuhakikisha familia zetu zinasonga mbele zikiwa na maendeleo mazuri kuhakikisha hakuna mtoto atakae achwa nyuma katika maendeleo."NO CHILD LEFT BEHIND" .

Hayo yote yatafanikiwa kwa kuwa na SIASA SAFI NA UONGOZI BORA.MAENDELEO AU MABADILIKO HAYATOKEI KWA SIKU MOJA,JITIHADA ZETU TUKISHIRIKIANA NA SIASA SAFI NA UONGOZI BORA Tutafika tunapotaka, Dr. Magufuli alishatutangazia kabisa katika kampeni yake kwamba mama NTILIE hatalipa tena kodi, mara atakapokuwa madarakani,hivi tunahesabu siku ifike. 

Epuka Mchepuko Mama Samia atatupigania, simama katika nafasi hiyo, tusidanganyike na sauti zetu zisikike. 

Ni heshima kubwa CCM imetupa hiyo ikiwa ni sera mojawapo ya kumheshimu mwanamke, kwa kuwa mwanamke ni chombo muhimu sana katika jamii.  

Mheshimiwa Rais  Mmtarajiwa alilitafakari kwa makini pamoja na uongozi wote wa CCM kuona kwamba inafaa tuangalie wanawake hu sio mwanzo ndani ya CCM wanawake tuna nafasi mbalimbali.

Lakini hii ya sasa hivi ni nafasi ya juu sana, utetezi na maamuzi mazuri tutayaona, hivyo basi acha MCHEPUKO CHAGUA MAGUFULI Siku ya mwisho utasema nilisimama katika nafasi yangu ndani ya jamii kwa kupiga kura na sasa hakuna mtoto anaeachwa nyuma kimaendeleo na matunda ndani ya jamii yanaonekana. ".WOMEN AS WINNERBREAD" CHAGUA DR. MAGUFULI CHAGU MAMA SAMIA.

No comments: