Monday, September 7, 2015

BENKI YA TIB YASAINI MKATABA WA KIUTENDAJI NA SERIKALI

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki ya Maendeleo TIB Prof. William Lyakurwa (wapili kushoto) na Msajili Hazina Bw. Lawrence Mafuru (wa pili kulia) wakibadilishana mikataba ya makubaliano ya kiutendaji kwenye hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.Mkataba huo unalenga kufungua milango kwa serikali kuweza kusimamia na kukagua ufanisi wa benki hiyo katika kuleta tija kwa taifa. Wanaoshuhudia ni pamoja na Msajili Hazina msaidizi Bw. Mwakibinga Mihalale (wa pili kulia) na Mkurugenzi Mtenddaji wa benki
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki ya Maendeleo TIB Prof. William Lyakurwa (kushoto) na Msajili Hazina Bw. Lawrence Mafuru (kulia) wakionyesha mikataba ya makubaliano ya kiutendaji baina yao mara baada ya kuisaini kwenye hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.Mkataba huo unalenga kufungua milango kwa serikali kuweza kusimamia na kukagua ufanisi wa benki hiyo katika kuleta tija kwa taifa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki ya Maendeleo TIB Prof. William Lyakurwa (kushoto) na Msajili Hazina Bw. Lawrence Mafuru (kulia) wakibadilishana mikataba ya makubaliano ya kiutendaji kwenye hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.Mkataba huo unalenga kufungua milango kwa serikali kuweza kusimamia na kukagua ufanisi wa benki hiyo katika kuleta tija kwa taifa. 

Na Mwandishi wetu
BENKI ya Maendeleo TIB imesaini mkataba wa kiuetendaji na Serikali hatua inayofungua milango kwa serikali kuweza kusimamia na kukagua ufanisi wa benki hiyo katika kuleta tija kwa taifa. 

Kusainiwa kwa mkataba huo kunaifanya benki hiyo kuwa miongoni mwa mashirika na taasisi za awali kabisa za umma zilitoa fursa kwa serikali kuzikagua na kupima ufanisi wao kiutendaji kila mwaka kupitia msajiri wa hazina.

Akizungumza kwenye hafla fupi ya kusaini mkataba huo iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa juma lilipita, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo Prof. William Lyakurwa alisema hatua hiyo itaisadia kuongeza msukumo zaidi kwa benki hiyo kuweza kuweza kutimiza malengo yake na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

“Licha ya ukweli kuwa tumekuwa tukitimiza wajibu wetu siku zote kwa kuhakikisha kwamba tunatoa huduma kwa weledi na ufanisi zaidi  lakini tunaamini kuwa uwepo wa mkataba huu utasaidia kutusukuma zaidi na hatimaye si tu tufikie malengo yetu bali pia hata kupitiliza malengo tuliyojiwekea,’’ alisema.

Aliongeza kuwa  mkataba huo pia utaongeza ari kwa waafanyakazi wa benki hiyo kwa kuwa utawajengea dhana ya uwepo wa nguvu ya ziada inayowasukuma zaidi kukamilisha majukumu yao kwa wakati na kwa ufanisi zaidi sambamba na matumizi sahihi ya fedha zinazotengwa kwa ajili ya uendeshaji wa benki hiyo.

“Mkataba huu kwetu ni ushahidi kwamba tunatimiza wajibu wetu kwa uwazi na zaidi tupo tayari kupimwa kwenye hilo.Lengo ni kuwa miongoni mwa taasisi bora kabisa za fedha hapa nchini na ulimwenguni kwa ujumla,’’ alisema.

Akizungumza kwenye hafla hiyo Msajiri Hazina Bw Lawrence Mafuru alisema  mikataba ya aina hiyo inalenga kuisaidia  serikali kupunguza hasara kubwa ambayo imekuwa ikapata kutoka kwenye mashirika na taasisi za umma zinazoshindwa kujiendesha kwa ufanisi  unaotakiwa.

Alibainisha kuwa  mashirika na taasisi za umma nyingi hapa nchini zinashindwa kujiendesha kwa ufanisi  kwa kuwa  kuna ombwe la  ufuatiliaji wa utendaji na matumizi ya pesa zinazotengwa kwa ajili ya uendeshaji wa mashirika hayo.

Akizungumzia mikataba hiyo Bw Mafuru alisema  kuwa licha ya  utaratibu huo kuwa mgeni hapa nchini lakini unalenga  kutambua taasisi na mashirika ya umma yanayoshindwa kujiendesha kwa ufanisi sambamba na matumizi mabaya ya fedha  za umma ili kutoa fursa kwa serikali kufanya maamuzi sahihi kulingana na aina ya changamoto zinazoyakabili mashirika hayo.

“Tunaamini huu ni mwanzo mpya kwenye usimamizi wa mashirika na taasisi hizi za umma na zote zinatakiwa ziwe na mkataba wa aina hii na tutakuwa wakali tukibaini udhaifu wowote ikiwemo kuwachukulia hatua kali wale wote watakaobainika kuhusika na udhaifu huo,’’ alisema.

Pia alitoa wito kwa wanasiasa wakiwepo wabunge kujitoa kwenye bodi za mashirika mbalimbali ya umma ili kuondoa mgongano wa kimaslahi kwa kuwa wao wana jukumu la kukagua mashirika hayo kupitia kamati za bunge.

No comments: