Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la NYUMBU (Tanzania Automative Technology Centre) Brigedia Jenerali Anselim akiongea na waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu miradi mbalimbali iliyotekelezwa na shirika hilo inayodhamiria kuwawezesha wananchi kiuchumi ikiwemo utengenezaji wa matrekta madogo( power Tiller) ambayo yanalenga kumkomboa mkulima hapa nchini kwa kuondokana na matumizi ya jembe la makono.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la NYUMBU (Tanzania Automative Technology Centre) Brigedia Jenerali Anselim.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Luteni Kanali Juma Nkangaa Sipe akiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) umuhimu wa kutoa habari za kuelimisha kwa jamii hasa zitakazowawezesha kuwajengea uwezo wa kimaarifa na kuwainua kichumi kupitia elimu hiyo.
Mhandisi Mkuu Msanifu Albert Wikedzi akiwaonesha waandishi wa Habari (Hawapo pichani) aina mbalimbali za sanifu zinazofanyika katika shirika hilo, wakati wa ziara ya waandishi wa habari katika kiwanda hicho Mjini kibaha.
Mkuu wa Kitengo cha Usubiaji Mhandisi Anderson Ole Zakaria akiwaeleza waandishi wa habari namna kitengo hicho kinavyofanya kazi ili kukidhi mahitaji ya kiwanda ambapo alisema kitengo hicho kinayeyusha hadi tani 2.5 za chuma zinazotumika kutengeneza bidhaa mbalimbali zinazotoka katika shirika hilo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la NYUMBU (Tanzania Automative Technology Centre) Brigedia Jenerali Anselim akiwaonesha waandishi wa habari moja aina ya gari la kivita lililotengezezwa na shirika hilo.

PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO
No comments:
Post a Comment