Friday, June 26, 2015

SOLUTION BLOCKS YAANDAA MIKUTANO ILI KUKUTANISHA NGO’S,TAASISI ZA KIRAIA NA TAASISI ZA SERIKALI KWA KILA MWENZI.

Na Avila kakingo,Globu ya jamii.
 
KAMPUNI ya Solution BLOCKS ikishirikiana na kampuni ya Anglo Gold Ashanti waandaa mkutano wa  Alhamisi ya kila mwezi ili kushirikisha taasisi mbalimbali za serikali na zisizo za kiserikali kuzungumzia kuchangia katika maendeleo katika  jamii.

Hayo yamesemwa na Makamo wa Rais wa Sustainability Aglo Gold Ashanti, Simon Shayo katika ufunguzi wa mkutano ambao umejulikana kwa jina la THURSDAY TALK  uliofanyika katika hoteli ya Colosseum  jijini Dar es Salaam jana.

  Nae Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Solution Blocks (Facilitator), amesema kuwa Makampuni na taasisi mbalimbali za kiserikali na zisizo za kiserikali lazima ziwajibike na kuelemisha jamii pia na kutoa fursa kwa wadau wa maendeleo hapa nchini ili kushiriki vyema katika kuleta maendeleo.

Pia ametoa wito kwa makampuni, NGO, taasisi za Serikali pamoja na Asasi za kiraia kuwajibika kushiriki vyema katika  kuleta maendeleo ya elimu,Afya,mazingira, maji pamoja na utawala bora katika taasisi hizo.

Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Solution Blocks, Msomisi Mbenna akizungumza katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Colosseum jijini Dar es Salaam jana.
 Makamu wa Raisi-Sustainability Anglo Gold Ashanti-Mgodi wa Geita,, Simon Shayo akizungumza na wadau waliohudhuria katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Colosseum jijini Dar es Salaam jana kuhusiana na mgodi wa dhahabu wa Geita jinsi unavyofanya kazi zake na kulinda afya za wananchi wa maeneo hayo ili wasidhurike na uchimbaji wa madini hayo.
Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa Anglo Gold Ashanti -Mgodi wa Geita, Tenga .M. Tenga akizungumza katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Colosseum jijini Dar es Salaam jana ulioandaliwa na kampuni ya Solution Blocks.
Baadhi ya wadau waliohudhuria katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Colosseum jijini Dar es Salaam jana kampuni ya Solution Blocks.
Kutoka kushoto ni Makamu wa Rais-Sustainability Anglo Gold Ashanti, Simon Shayo, Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Solution Blocks, Msomisi Mbenna na Afisa uhusiano na mawasiliano wa Anglo Gold Ashanti -Mgodi wa Geita, Tenga .M. Tenga.

Kutoka kushoto ni Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa Anglo Gold Ashanti -Mgodi wa Geita, Tenga .M. Tenga, Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Solution Blocks, Msomisi Mbenna na Afisa mahusiano na mawasiliano wa Benjamini Mkapa  HIV/AIDS Foundation, Deogratius Rimoy wakiwa katika picha ya pamoja katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Colosseum jijini Dar es Salaam jana.

Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

No comments: