Monday, June 8, 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA TAMASHA LA BULABO KABILA LA WASUKUMA MKOANI MWANZA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na Mwenyekiti wa Machifu wa Kisukuma Charles llago Kaphipa wakati wa sherehe za Kimila za wasukuma kwenye Tamasha la bulabo katika kituo cha bujoro Mkoani Mwanza Jana Tarehe 7/6/2015.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohammed Ghar Bilal akishika jiwe la kutengenezea chuma wakati wa Uchifu kulia ni Mkurugenzi wa kituo cha Bujora Askofu Fabian Mkoja alipotembelea Maonyesho hayo Kijiji cha Kisesa wilaya ya Magu Mkoa wa Mwanza jana tarehe 7/6/2015.
Makamuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohammed Gharib Bilal akipata maelezo toka kwa Mkurugenzi wa kituo cha Bujora Askofu Fabian Mkoja alipotembelea Nyumba ya Mtemi wa kabila la wasukuma kwenye kituo cha Bujora Mkoani Mwanza jana Tarehe 7/6/2015.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohammed Gharib Bilal akiwapungia Mkono wananchi wa Kijiji Cha Kasesa wilaya ya Magu wakati alipowasili Uwanjani hapo kuzindua Tamasha la Kimila la wasukuma Mkoa wa Mwanza jana Tarehe 7/6/2015.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohammed Gharib Bilal akihutubia Wananchi wa Kijiji cha kisesa Wilaya ya Magu,katika sherehe za Kimila ya wasukuma zilizofanyika Mkowani Mwanza jana tarehe 7/6/2015.
Makamu wa Raiswa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohammed Gharib Bilal akipiga Ngoma ishara ya Kuzindua Sherehe za kimila za kabila la wasukuma zilizofanyika kwenye kijiji cha kisesaWilayani Magu Mkoa wa Mwanza jana.PICHA NA OMR.

No comments: