Wednesday, June 10, 2015

MAFURIKO YA LOWASA YATIKISA MKOA WA MARA

Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, akipungia mkono maelfu ya wana CCM na wananchi wa Musoma, alipowasili uwanja wa ndege wa Musoma Juni 9, 2015, kuendelea na kampeni yakle ya kuomba wana CCM wamdhamini baada ya kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa na CCM kuwania nurais wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015

Lowassa, (kulia), akiwatuliza wana CCM na wananchi wa Musoma, waliojaribu kuvunja geti ili walao wapate kugusana naye alipowasili uwanja wa ndege wa Musoma, Juni 9, 2015, kwa nia yabkuomba wana CCM wamdhamini

Wana CCM na wananchi wa Musoma, wakipiga kelele kumwita Mh. Lowassa, ili awasogelee kumsalimia huku wakiwa nje ya geti la uwanja wa ndege wa Musoma

Mh. Lowassa, akiongea na bibi kizee huyu aliyeomba walau amshike mkono ili kumpa baraka katika safari yake ya matumaini 2015, alipowasili kwenye ofisi za CCM wilaya ya Bunda, mkoani Mara, Juni 9, 2015 kuomba wana CCM wamdhamini

Mh. Lowassa, akiwasili ofisi za CCM wilaya ya Bunda

Mh. Lowassa, (kushoto), akiwashukuru wana CCM na wananchi waliojitokeza kwenye ofisi za CCM wilaya ya Bunda, wengine kwa nia ya kumdhamini na wengine kumuona

Umati wa watu uliofurika kwenye ofisi za CCM wilaya ya Bunda, huku wengine wakiwa juu ya mti walau wapate kumuona

Mh. Lowassa a,kiwasili ofisi za CCM wilaya ya Musoma

Mh. Lowassa akiwasili ofisi za CCM, wilaya ya Tarime mkoani Mara

Mh. Lowassa mkiwapungia wana CCM na wananchi wengine alipowasili ofisi za CCM, wilaya ya Tarime

Msanii huyu yeye aliamua kuja na ritungu huko Rorya wakati Mh. Lowassa a.lipowasili ofisi za CCM wilaya ya Rorya


No comments: