Sunday, May 31, 2015

KAMPENI YA KUTOKOMEZA MARADHI YA FISTULA YATUA WILAYA YA KIBONDO

Mkazi wa Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma Esther Batolomea akisoma kipeperushi chenye ujumbe wa maradhi ya Fistula wakati wa kampeni ya kutokomeza maradhi hayo iliyofanyika wilayani hapo. Hospitali ya CCBRT kwa kushirikiana na Vodacom Foundation zinatoa elimu kwa Umma kupitia kampeni inayozunguka mikoa mitatu nchini kuwasisitiza wanawake wajitokeze wakatibiwe maradhi hayo kwani yanatibika. Inakadiriwa wastani ya wanawake 3,000 hupatwa na maradhi hayo kwa mwaka wakati wa kujifungua.
Wakazi wa Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma wakisoma vipeperushi vyenye ujumbe wa maradhi ya Fistula wakati wa kampeni ya kutokomeza maradhi hayo iliyofanyika wilayani hapo. Hospitali ya CCBRT kwa kushirikiana na Vodacom Foundation zinatoa elimu kwa Umma kupitia kampeni inayozunguka mikoa mitatu nchini kuwasisitiza wanawake wajitokeze wakatibiwe maradhi hayo kwani yanatibika. Inakadiriwa wastani ya wanawake 3,000 hupatwa na maradhi hayo kwa mwaka wakati wa kujifungua.
Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Kumwamba iliyopo Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma walijumwika na wakazi wa wilaya hiyo katika viwanja vya Community Centre wakimsiliza Meneja Biashara wa Idara ya Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Grace Lyon wakati alipokuwa akiwafafanulia jambo kuhusiana na maradhi ya Fistula. Wakati wa kampeni ya kutokomeza maradhi hayo inayoendelea kufanyika katika mikoa mitatu nchini,Kampeni hiyo inaendeshwa na Hospitali ya CCRBT kwa kushirikiana na Vodacom Foundation. Inakadiriwa wastani ya wanawake 3,000 hupatwa na maradhi hayo kwa mwaka wakati wa kujifungua.
Balozi wa maradhi ya Fistula nchini Msanii Mrisho Mpoto alimaarufu”Mjomba” akitoa elimu kwa wakazi wa Kibonda kuhusiana na maradhi ya fistula na kuwasihi wakina baba kuwaruhusu wake zao wakatibiwe maradhi hayo kwani yanatibika. Alitoa elimu hiyo wakati wa kampeni inayoendeshwa na Vodacom Foundation kwa kushirikiana na CCBRT ya kutokomeza maradhi hayo inayoendelea katika mikoa mitatu nchini. Inakadiriwa wastani wa wanawake 3,000 hupatwa na maradhi hayo kwa mwaka wakati wanapojifungua.

No comments: