Wednesday, April 22, 2015

Maonesho ya Nne ya Vito ya Arusha

 Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara wa Madini ya Vito nchini (TAMIDA), Sammy Molel (aliyesimama), akiwaeleza Wafanyabiashara wa madini hayo utaratibu wa kushiriki katika Maonesho ya Nne ya Vito ya Arusha. Maonesho hayo yanafanyika katika Hoteli ya Mount Meru  jijini humo katika Hoteli ya Mount Meru kuanzia Aprili 21 – 24, 2015.
 Baadhi ya Wafanyabiashara wa madini ya vito nchini, wakimsikiliza Mwenyekiti wao, Sammy Molel (hayupo pichani) aliyekuwa akiwaeleza utaratibu wa kushiriki katika Maonesho ya Nne ya Vito ya Arusha. Maonesho hayo yanafanyika katika Hoteli ya Mount Meru
 Baadhi ya Wafanyabiashara wa madini ya vito nchini, wakimsikiliza Mwenyekiti wao, Sammy Molel (hayupo pichani) aliyekuwa akiwaeleza utaratibu wa kushiriki katika Maonesho ya Nne ya Vito ya Arusha. Maonesho hayo yanafanyika katika Hoteli ya Mount Meru
 Baadhi ya Wanakamati/Sekretarieti ya Maandalizi ya Maonesho ya Nne ya Vito ya Arusha, wakiwa katika hatua za mwisho za maandalizi katika Hoteli ya Mount Meru.

 Maandalizi ya Maonesho: Sekretarieti wakiwasajili washiriki mbalimbali wa Maonesho ya Vito ya Arusha yanayofanyika katika Hoteli ya Mount Meru jijini humo. Maonesho hayo yatafunguliwa rasmi Aprili 22 na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene.

 Maandalizi ya Maonesho: Sekretarieti wakiwasajili washiriki mbalimbali wa Maonesho ya Vito ya Arusha yanayofanyika katika Hoteli ya Mount Meru jijini humo. Maonesho hayo yatafunguliwa rasmi Aprili 22 na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene.

 Maandalizi ya Maonesho: Sekretarieti wakiwasajili washiriki mbalimbali wa Maonesho ya Vito ya Arusha yanayofanyika katika Hoteli ya Mount Meru jijini humo. Maonesho hayo yatafunguliwa rasmi Aprili 22 na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene.

 Kamishna Msaidizi wa Madini, Sehemu ya uongezaji thamani madini, Salim Salim (kushoto) akitoa maelezo kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha Jowika Kasunga (katikati) kuhusu madini vito, alipotembelea maonesho ya vito ya Arusha yanayofanyika katika Hoteli ya Mount Meru jijini humo. Hili ni moja ya mabanda katika maonesho hayo.

 Wafanyabiashara wa madini ya vito wakiuza madini kwa wateja. Hili ni moja ya mabanda katika maonesho ya vito ya Arusha yanayofanyika katika Hoteli ya Mount Meru jijini humo.

 Wafanyabiashara wa madini vito wakitathmini madini yao kabla ya kuyapanga tayari kwa mauzo katika maonesho ya vito ya Arusha. Maonesho hayo yanafanyika katika Hoteli ya Mount Meru jijini humo
 Wafanyabiashara wa madini ya vito kutoka Rwanda wakimpatia Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Jowika Kasunga na ujumbe wake vijitabu vyenye maelezo kuhusu madini hayo, alipotembelea banda lao katika maonesho ya vito yanayoendelea jijini Arusha katika Hoteli ya Mount Meru. 
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Jowika Kasunga (kulia-katikati), akiangalia kinyago cha Ndege aliyetengenezwa kwa kutumia jiwe, alipotembelea banda la Kituo cha Jimolojia Tanzania. Kituo hicho hutoa mafunzo ya ukataji madini ya vito pamoja na uongezaji thamani mawe. 
 Afisa Uhusiano Wakala wa Ukaguzi Madini Tanzania (TMAA), Yisambi Shiwa (Kulia), akitoa maelezo kuhusu huduma zinazotolewa na Wakala huo kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Jowika Kasunga na ujumbe wake, alipotembelea banda la TMAA katika maonesho ya vito ya Arusha yanayofanyika jijini humo katika Hoteli ya Mount Meru kuanzia Aprili 21 – 24, 2015.

 Maandalizi ya Maonesho: Sekretarieti wakiwasajili washiriki mbalimbali wa Maonesho ya Vito ya Arusha yanayofanyika katika Hoteli ya Mount Meru jijini humo. Maonesho hayo yatafunguliwa rasmi Aprili 22 na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene.

 Baadhi ya madini ya vito yanayouzwa na wafanyabiashara wa madini hayo katika maonesho ya vito ya Arusha, yanayofanyika jijini humo katika Hoteli ya Mount Meru kuanzia Aprili 21 – 24, 2015. Maonesho hayo yatafunguliwa rasmi Aprili 22 na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene.
  Baadhi ya madini ya vito yanayouzwa na wafanyabiashara wa madini hayo katika maonesho ya vito ya Arusha, yanayofanyika jijini humo katika Hoteli ya Mount Meru kuanzia Aprili 21 – 24, 2015.
  Baadhi ya madini ya vito yanayouzwa na wafanyabiashara wa madini hayo katika maonesho ya vito ya Arusha, yanayofanyika jijini humo katika Hoteli ya Mount Meru kuanzia Aprili 21 – 24, 2015.
 Baadhi ya madini ya vito yanayouzwa na wafanyabiashara wa madini hayo katika maonesho ya vito ya Arusha, yanayofanyika jijini humo katika Hoteli ya Mount Meru kuanzia Aprili 21 – 24, 2015.

No comments: