Thursday, March 19, 2015

WATOTO ZAIDI YA ELFU KUMI HUZALIWA NA SIKO SELI KILA MWAKA NCHINI

Mratibu wa Mradi wa MDOTS unoafanya utafiti wa tiba ya ugonjwa wa siko seli (Sickle Cell) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Robert Mongi (kulia) akifafanua jambo kwa baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania waliofika hospitalini hapo kukabidhi msaada wa simu 150 aina ya ZTE zitakazotumiwa na wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo.
Mkuu wa kitengo cha Vodacom Foundation Reenu Verma (kulia) akimfungulia boksi lenye moja ya simu kati ya 150 aina ya ZTE, Mratibu wa Mradi wa MDOTS unoafanya utafiti wa tiba ya ugonjwa wa siko seli (Sickle Cell) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt Robert Mongi wakati wa makadhiano ya msaada wa simu hizo zilizotolewa na mfuko huo kwa ajili ya wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo.
Mkuu wa kitengo cha Vodacom Foundation Reenu Verma (kushoto) akimkabidhi boksi lenye simu 150 aina ya ZTE, Mratibu wa Mradi wa MDOTS unoafanya utafiti wa tiba ya ugonjwa wa siko seli (Sickle Cell) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt Robert Mongi, Kwa niaba ya wagonjwa wa sikoseli msaada wa simu hizo zilizotolewa na mfuko (Vodacom Foundation) kwa ajili ya wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo.
Mtoto Nira Khamis (12) anayesumbuliwa na Ugonjwa wa Siko Seli akionesha simu aina ya ZTE ambayo atatumia kwa ajili ya kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa. Jumla ya simu 150 zimetolewa msaada na Vodacom Foundation katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo. Wanaoshuhudia katika picha ni mkuu wa kitengo cha Vodacom Foundation Reenu Verma (kushoto) na Mratibu wa matibabu kwa njia ya teknolojia Dkt . Deogratius Soka.
Mkuu wa kitengo cha Vodacom Foundation Reenu Verma (kushoto)akimkabidhi moja ya simu kati ya simu 150 aina ya ZTE, Mtoto Nira Khamis(12) anayesumbuliwa na ugonjwa wa Siko Seli ambayo atatumia kwa ajili ya kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa. Jumla ya simu 150 zimetolewa msaada na Vodacom Foundation katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakiwa wamebeba maboksi yenye simu aina ya ZTE walipofika kukabidhi msaada wa simu 150 zilizotolewa msaada na Vodacom Foundation katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakiwa wamepozi kwa picha kabla ya kukabidhi msaada wa simu 150 zilizotolewa msaada na Vodacom Foundation katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo.

Tatizo la Ugonjwa wa Siko Seli ni kubwa nchini na limekuwa likiongezeka kila mwaka ambapo hadi kufikia sasa watoto wapatao 11,000 nchini wanazaliwa wakiwa na ugonjwa huu hatari ambao husababisha upungufu wa damu mwilini.

Hayo yamebainishwa na Dk Robert Mongi ambaye ni mratibu wa kitengo cha Siko Seli kwa watoto katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakati wa kupokea msaada wa simu 150 za mkononi kwa ajili ya  kuratibu matibabu ya wagonjwa wanaotibiwa kwenye kitengo hicho zilizotolewa na kampuni ya Vodacom kupitia taasisi yake ya kusaidia masuala ya  jamii ya Vodacom Foundation.

Dk. Mongi alisema tatizo la ugonjwa huu ni kubwa na unatibika iwapo mgonjwa atapima na kuanza kutumia madawa mapema ikiwemo kuzingatia masharti anayopaswa kufuata mgonjwa.

Alisema hivi sasa vipimo vya ugonjwa huu vinapatikana katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili tu ,hali ambayo inasababisha waathirika wa ugonjwa huu wanaoishi nje ya mkoa wa Dar es Salaam kuchelewa kupata vipimo na wengi wao kupoteza maisha.”Kutokuwepo na mashine za kufanyia kipimo cha ugonjwa huu za kutosha ni moja ya changamoto kubwa inayokwamisha kuutokomeza kwa kuwa kuna idadi kubwa ya wagonjwa sehemu mbalimbali za nchi wanashindwa kufanya vipimo na kuugundua ugonjwa mapema ili waanze kutumia dawa”.Alisema

Aliishukuru Vodacom Foundation kwa msaada huo wa simu  ambao alisema utawafikia walengwa ambao ni wagonjwa wanaotumia dawa na zitasaidia kuratibu matibabu yao kwa  kupigwa picha  wanapokuwa wanameza dawa wakiwa  majumbani kwao na picha hizo kuwasilishwa hospitalini hapo kwa ajili ya kuwekwa kwenye  mfumo wa kumbukumbu za matibabu ya wagonjwa.

Akiongea muda mfupi baada ya kukabidhi msaada huo Meneja wa Ruzuku na Mawasiliano wa Vodacom Foundation Renatus Rwehikiza ambaye aliambatana na baadhi ya wafanyakazi  wa Vodacom alisema kampuni ya Vodacom kupitia taasisi yake ya Vodacom Foundation imeona kuna  umuhimu wa kuwapatia wagonjwa simu ili ziwasaidie wakati wa matibabu yao.

“Tunajua kuwa kuna makundi mengi ya wahitaji katika jamii hivyo tumeona safari hii tuangalie kundi la wagonjwa  wanaotibiwa Siko Seli kwa kuwa ugonjwa huu unazidi kuongezeka na unahitaji jitihada za ziada kutoka kwa wadau mbalimbali katika kuutokomeza”.Alisema Rwehikiza.


Vodacom kupitia taasisi yake ya Vodacom Foundation imekuwa ikitoa  misaada mbalimbali ya kuleta mabadiliko kwenye jamii hususan katika sekta ya elimu na Afya bila kusahau makundi yenye mahitaji maalumu kwenye jamii.

No comments: