Saturday, March 21, 2015

MAMA SALMA KIWETE AKABIDHI GARI LA WAGONJWA KWENYE HOSPITALI YA MKOMAINDO HUKO MASASI

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na mmoja wa wauguzi katika hospitali ya Wilaya ya Masasi, Mkomaindo, mara baada ya kuwasili hospitalini hapo kwa ajili ya kuwatembelea wagonjwa tarehe 19.3.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimwelekeza Bibi Zauda Amuli,18, mkazi wa Mtaa wa Moroco namna ya kumnyonyesha mtoto wake mchanga aliyezaliwa tarehe 17.3.2015 katika hospitali ya Mkomaindo huko Masasi tarehe 19.3.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimchukua mtoto mchanga kutoka kwa mama yake Bibi Malisela Amandus, 24, anayeishi mtaa wa Silabu huko Masasi wakati Mama Salma alipotembelea hopitalini hapo kuwajulia hali wagonjwa tarehe 19.3.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Ndugu Halima Dendegu (kushoto) na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkomaindo Dkt. Musa Rashid (kulia) wakitembelea maeneo mbalimbali ya hospitali hiyo.
Mama Salma Kikwete, Mke wa Rais akiwasalimia wazee wa Mji wa Masasi wakati alipowasili kwenye eneo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Masasi kwa ajili ya kukabidhi gari la wagonjwa kwenye hospitali ya Wilaya, Mkomaindo, tarehe 19.3.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwasslimia wanafunzi waliofika kwenye sherehe ya kukabidhi gari la wagonjwa (ambulance) kwenye Hospitali ya Wilaya ya Masasi, Mkomaindo, tarehe 19.3.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wananchi wa Masasi waliohudhuria sherehe ya kukabidhi gari la wagonjwa (ambulance) kwenye Hospitali ya Mkomaindo huko Masasi tarehe 19.3.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikabidhi kadi ya gari la wagonjwa (ambulance) kwa Meya wa Mji wa Masasi Mheshimiwa Andrew Mtumsha kwenye sherehe iliyofanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Masasi tarehe 19.3.2015. Aliyesimama kulia kwa Mama Salma ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wa Mkoa wa Mtwara Ndugu Mohamed Sinani na kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ni Ndugu Halima Dendegu.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na serikali kuangalia sehemu ya ndani ya gari la kubebea wagonjwa lililokabidhiwa kwenye hospitali ya Mkomaindo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiagana na wananchi mbalimbali kwa kuwapungia mikono baada ya kukamilisha zoezi la kukabidhi gari la wagonjwa kwenye hospitali ya Mkomaindo huko Masasi tarehe 19.3.2015. PICHA NA JOHN LUKUWI.

No comments: