Friday, February 6, 2015

ZIMAMOTO WA JIJI LA LINZ, AUSTRIA WATEMBELEA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Juma Malemi akiongoza kikao wakati Viongozi wa Kikosi cha Zimamoto toka Jiji la Linz, Austria walipotembelea Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji cha Jiji la Linz, Austria Christian Puchner, akimkabidhi Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Juma Malemi mojawapo ya kofia za zimamoto zilizotolewa kama msaada kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji la Tanzania. Kushoto ni Diwani wa Jiji la Linz Bwana Deltef Wimmer.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Juma Malemi akijaribisha mojawapo ya kofia za zimamoto zilizotolewa na Jeshi la Zimamoto la Jiji la Linz, Austria kama msaada kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji la Tanzania.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Juma Malemi katika picha ya pamoja na ujumbe wa Kikosi cha Zimamoto toka Linz, Austria waliotembelea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Juma Malemi akiagana na Diwani wa Jiji la Linz, Austria, Deltef Wimmer, baada ya ujumbe wa Kikosi cha Zimamoto cha Jiji la Linz kumaliza ziara yao katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Bwana Wimmer alikuwa kiongozi wa ujumbe huo.
Ujumbe wa Kikosi cha Zimamoto toka Jiji la Linz, Austria, wakifurahia mazingira ya Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi baada ya kumaliza ziara yao wizarani hapo.

No comments: