Thursday, January 1, 2015

SIKU YA PILI ILIVYOKUWA KWA MABALOZI WAKATI WAKIPANDA MLIMA KILIMANJARO

Majira ya saa moja asubuhi katika kituo cha Mandara ikiwa ni siku ya pili ya safari ya Mabalozi kupanda Mlima Kilimanjaro maandalizi ya muendelezo wa safari hiyo yanaanza.
Balozi wa Tanzania katika falme za nchi za kiarabu,Mbarouk N. Mbarouk akiongoza msafara wa Mabalozi kuelekea kituo cha Horombo.
Safari inaendelea.
Balozi Adadi Rajab anayeiakilisha Tanzania nchini  Zimbabwe na Mauritius akitafakari safari ya kuelekea kituo cha Horombo.
Mabalozi Patrick Tsere (Malawi) na Balozi Batilda Burian wakivuta pumzi kwanza kabla ya kuendelea na safari.
Balozi Grace Mujuma (Zambia) akiongozana na Balozi Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB),Balozi Charles Sanga wakienda na mwendo wa Mdogo mdogo.
Muongoza watalii mkuu msaidizi wa kampuni ya Zara Tour,Theofiri(mwenye miwani) akiwaongoza mabalozi kuelekea kituo cha Horombo.
Mabalozi ,Waandishi pamoja na waongoza watalii wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutembea kwa umbali mrefu kueleka Horombo.
Safari ya kuelekea kituo cha Horombo ikaendelea kwa pamoja bila ya kuacahana.
Mahala pengine Mabalozi walilazimika kutumia fimbo maalumu kupanda maeneo ambayo yalkuwa na vipando vikali.
Mabalozi ,Shamim Nyanduga( Msumbiji) na Radhia Msuya (Afrika Kusini) walilazimika kupaka mafuta mgando katika nyuso zao ili kuzuia kubabuka na jua.
Balozo Tsere akipatiwa huduma ya kwanza ya kuchuwa mguu wake ili aweze kuendelea na safari ,kulia ni balozi Batilida Buriani.
Balozi Mwinyi aliamua kupoza koo huku akitafakari safari hiyo.
Kila mmoja aliamua kupumzika ili kuvuta nguvu ya kumalizia kipande kilichokuwa kimebakia.
Maeneo mengine mabalozi walifanya mazungumzo na wageni waliokuwa wakishuka toka kileleni.
Hatimaye Mabalozi wakafika eneo la nusu njia kuelekea Horombo na kupata chakula .
Wale waliokuwa wamepungukiwa maji waliongezewa kwa kuwa ndio dawa pekee ili kufanikisha kuwez kupanda Mlima Kilimanjaro.
Safari ikaendelea.
Hataimaye kituo cha Horombo kikaonekana kwa mbali na mabalozi walitembea na kupumzika hapo.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya jamii kanda ya kaskazini aliyekuwa katika msafara wa Mabalozi kupanda Mlima Kilimanjaro.

No comments: