Monday, January 5, 2015

BENKI YA AZANIA TAWI LA MOSHI, YAWAANDALIA WATEJA WAKE NA WAFANYAKAZI PARTY YA KUUKARIBISHA MWAKA MPYA

Wafanyakazi wa Benki ya Azania Tawi la Moshi, wakiwa wamejumuika katika sherehe ya kupongezana kwa mafanikio waliyoyapata katika mwaka ulioisha wa 2014 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2015. Sherehe hiyo ilifanyika jana katika Benki hilo, lililoko, mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Meneja wa Benki ya Azania Tawi la Moshi, Bi.Hajira Mmambe, akifungua zawadi katika hafla ya kuuaga mwaka 2014 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2015 iliyofanyika jana kama sehemu ya kuwapongeza wafanyakazi wa Benki hiyo.  
Meneja wa Benki Tawi la Moshi, Bi. Hajira Mmambe akishiriki kuwaandalia wateja chai, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa Benki hiyo kujumuika na wateja wake katika Sherehe za kuuaga Mwaka na kuukaribisha mwaka mpya.
Bi. Hajira akiendelea na zoezi la kuwahudumia wateja kifungua kinywa
Hapa mmoja wa wateja akipokea Keki kutoka kwa Meneja wa Benki la Azania tawi la Moshi, Bi. Hajira Mmambe (wa pili kushoto)
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya Kasakazini

No comments: