Saturday, December 13, 2014

RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA PIL,ALHAJ MWINYI ATEMBELEA MIRADI MBALIMBALI YA NSSF JIJINI DAR LEO

Rais Mstaafu wa awamu ya pili nchini Tanzania,Alhaj Ali Hassan Mwinyi ametembelea miradi mbalimbali ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ambapo aliweza kutembelea na kuangalia maendeleo ya ujenzi wa daraja la Kigamboni, daraja ambalo linategemea kukamilika mwezi wa saba mwaka 2015 na vilevile amepata nafasi ya kutembelea Ujenzi wa nyumba za shirika la NSSF ambao unaendelea katika eneo la Mtoni Kijichi Kigamboni na baadhi ya nyumba hizo zimeishauzwa. Pia Rais Mstaafu aliweza kutembelea ujenzi wa mji mpya wa Dege uliopo eneo la Kigamboni jijini Dar.

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Injinia Abubakar Rajabu akifafanua jambo baada ya Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi kufanya ziara ya kutembelea ujenzi wa Daraja la Kigamboni,Nyumba za Mtoni Kijichi na Ujenzi wa mji mpya wa Dege.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dk. Ramadhan Dau (wa kwanza kulia) akimweleza jambo Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi alipofanya ziara yake kuona ujenzi mkubwa unaodhaminiwa na NSSF
WaziriI wa Kazi na Ajira, Mh. Gaudentia Kabaka  akimkaribisha Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi  alipofanya ziara yake kwenye mirandi mbalimbali ya maendelea inayodhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)
Meneja Mradi Mhandisi Karim Mataka akitoa ufafanuzi wa ujenzi wa Daraja la Kigamboni
Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi akifuatilia kwa umakini
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dk. Ramadhan Dau akitoa ufafanuzi kwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi kuhusu daraja la Kiganboni
Ufafanuzi ukitolewa na Meneja Mradi wa Daraja la Kigamboni Mhandisi Karim Mattaka.
Wafanyakazi wakiendelea na ujenzi wa Daraja la Kigamboni
Meneja Mradi wa Daraja la Kigamboni Mhandisi Karim Mattaka akitoa ufafanuzi
Hii ni moja ya nguzo ambayo daraja hilo la kigamboni litakapopita
Injinia Julius Nyamhokya akitoa ufafanuzi  kwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi kuhusu ujenzi wa nyumba za Mtoni Kijichi/Kigamboni ambazo zimejengwa kwa hisani ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)
Hizi ni baadhi ya nyumba zilizoko kwenye awamu ya mwisho ya ujenzi
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dk. Ramadhan Dau akitolea ufafanuzi wa moja ya majengo hayo 
Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi akikagua ujenzi wa mji mpya wa Dege
Injinia Julius Nyamhokya akitoa ufafanuzi kuhusu vifaa vingi vinavyotumika kwenye ujenzi huo vinatengenezwa ndani ya viwanda ambavyo vimo ndani ya mradi kwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi 
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dk. Ramadhan Dau akieleza jambo kwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi 
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dk. Ramadhan Dau  akitoa ufafanuzi kwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi kuhusu jengo litakalotumia kuuzia nyumba pamoja na kusimamia nyumba zote zitakazo kuwa kwenye eneo la Dege
Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi akizungumza na vyombo vya habari mara baadaya kumaliza ziara yake iliyoanzia kwenye Daraja la Kigamboni, Nyumba za Mtoni Kijichi pamoja na ujenzi wa mji mpya wa Dege.
Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi akiagana na WaziriI wa Kazi na Ajira,Mh. Gaudentia Kabaka mara baada ya kumaliza ziara yake wa pili kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dk. Ramadhan Dau
Huu ndio mwonekano halisi wa mji mpya wa Dege utakaokuwa Kigamboni

No comments: