Monday, December 1, 2014

BODI YA KAHAWA NCHINI (TCB) YAZINDUA MTAALA ENDELEVU WA KITAIFA JUU YA ZAO LA KAHAWA NCHINI

Mtafiti mafunzo, usambazaji na teknolojia kutoka taasisi ya utafiti wa zao la Kahawa (TACri),Jeremia Magesa (kulia) na Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Kahawa Kajiru Kisenge wakifuatilia mawasilisho yaliyokuwa yakifanywa na mwakilishi wa Cafe Africa ,Catherine Mwangata(Hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa mtaala endelevu wa kitaifa juu ya zao la Kahawa nchini.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Bodi ya Kahawa Tanzania(TCB) Astery Bitegeko akipitia mambo kadhaa yaliyokuwa yakiwasilishwa wakati wa uzinduzi wa mtaala endelevu wa kitaifa juu ya zao la Kahawa ,uzinduzi uliofanyika katika ukumbi wa mikutano ya Bodi ya TCB,kulia kwake ni afisa utumishi wa TCB,Moses Chimwinga.
Wawakilishi wa Cafe Africa,Catherine Mwangata(Coutry Manager)  na Wiliam Wakuganda(Special Advisor) wakifuatilia mjadala wakati wa uzinduzi wa mtaala endelevu wa kitaifa juu ya zao la Kahawa ,uzinduzi uliofanyika katika ukumbi wa mikutano ya Bodi ya TCB.
Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Bodi ya Kahawa Tanzania(TCB) Alhaj ,Dk Juma Ngasongwa(shoto) akiwa na Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Kahawa Tanzania(TCB0 Adolf Kumburu wakifuatilia kwa makini maelezo ya mwakilishi wa Cafe Africa hayupo pichani.
Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Bodi ya Kahawa Tanzania(TCB) Alhaj Dk Juma Ngasongwa akichangia wakati wa uzinduzi wa mtaala endelevu wa kitaifa juu ya zao la Kahawa.
Mtafiti mafunzo, usambazaji na teknolojia kutoka taasisi ya utafiti wa zao la Kahawa (TACri),Jeremia Magesa akichangia jambo wakati wa uzinduzi wa mtaala endelevu wa kitaifa juu ya zao la Kahawa.
Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Kahawa Tanzania(TCB) Adolf Kumburu akitoa neno wakati wa uzinduzi wa mtaala endelevu wa kitaifa juu ya zao la Kahawa ,uzinduzi uliofanyika katika ukumbi wa mikutano ya Bodi ya TCB.
Mwakilishi wa Cafe Africa nchini Tanzania ,Catherine Mwangata akifafanua jambo wakati akiwasilisha mtaala endelevu wa kitaifa juu ya zao la Kahawa uliozinduliwa na Bodi ya Kahawa nchini (TCB). Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya Kaskazini.

No comments: