Sunday, November 16, 2014

Wabunge washiriki zoezi la kupima afya zao mjini Dodoma

Waziri wa Afya Mhe.Dkt Seif Rashidi aongoza zoezi la kupima afya za Wabunge katika Ukumbi wa Msekwa jana.Upimaji wa afya za Wabunge umefanywa na Madaktari wa Aga Khan kutoka Morogoro,Dar. na Dodoma.
Waziri wa Afya Mhe.Dkt Seif Rashidi (kulia) akisalimiana na Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya Agha Khan,Sisawo Konteh wakati wa zoezi la upimaji wa Afya kwa Waheshimiwa Wabunge,Mjini Dodoma jana.Katikani ni Mmoja wa Maafisa waandamizi wa Hospitali ya Agha Khan.
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini,Mchungaji Luckson Mwanjale akimsikiliza kwa Makini Mtaalam wa Maswala ya Afya kutoka Hospitali ya Agha Khan wakati wa zoezi la kupima Afya kwa waheshimiwa Wabunge,Mjini Dodoma jana.
Mh. Zakhia Meghji akipewa maelezo na Daktari Raheel Kanji wa Hospitali ya Agha Khan
Mh. Mbunge akifanyiwa vipimo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (kazi maalum),Prof. Mark Mwandosya akijiandaa kupima uzito wake.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma akipima akichukuliwa vipimo na Daktari kutoka Hospitali ya Agha Khan.
Ushauri.
Waziri wa Afya Mhe.Dkt Seif Rashidi akiongea na wanahabari juu ya zoezi la upimaji Afya kwa Waheshimiwa Wabunge aliloliongoza.
Waheshimiwa Wabunge wakiendelea kumiminika kwenye Ukumbi wa Msekwa,Bungeni Mjini Dodoma ili kushiriki zoezi la upimaji Afya.

Sehemu ya Waandishi wa Habari wakifatilia kwa makini zoezi hilo.Picha zote na Deusdedit Moshi,Globu ya Jamii,Kanda ya Kati.

No comments: