Friday, October 10, 2014

Wadau wa Vijana washiriki mdahala katika Wiki ya Vijana mkoani Tabora

Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Steven Kissuiakizungumza katika mdahalo wa vijana leo mkoani Tabora ambapo mdahalo huo umefanyika ikiwa ni kuadhimisha Wiki ya Vijana ambayo kitaifa inafanyika mkoani hapa.
Mchumi Mkuu Sekretariat ya Mkoa wa Tabora Bw.Nicholas Kileka akitoa mada kuhusu ijue Tabora leo mkoani humo wakati wa mdahalo uliohusisha vijana mbalimbali wanaoshiriki maadhimisho ya Wiki ya Vijana ambayo kitaifa yanafanyika mkoani humo.
Afisa Vijana Mwandamizi kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Florent Karist akitoa mada kuhusu maudhui ya Wiki ya Vijana leo mkoani humo wakati wa mdahalo uliohusisha vijana mbalimbali wanaoshiriki maadhimisho ya Wiki ya Vijana ambayo kitaifa yanafanyika mkoani humo.
Baadhi ya Washiriki wa mdahalo wa Vijana katika kuadhimisha Wiki ya Vijana wakichangia mada katika mdahalo huo leo mkoani Tabora.
Baadhi ya Washiriki wa mdahalo wa Vijana katika kuadhimisha Wiki ya Vijana wakifuatilia mada katika mdahalo huo leo mkoani Tabora. Picha na Frank Shija, WHVUM.

No comments: