Thursday, September 25, 2014

Kada Mzalendo Loveness Mamuya na Mrejesho wa Kwanini Usiku wa Jakaya ni Kitu cha Kujivunia Daima

1.   UTANGULIZI

Binadamu hakuumbwa katika ombwe, ameumbwa akiwa katika dimbwi la majukumu, kwake binafsi, familia, jamii na dunia kwa ujumla. Wachache sana wanaoweza kupitia ngazi zote za uwajibikaji huu. Katika hao wachache, hatutasita kumtaja Jakaya Khalifan Mrisho Kikwete. Ili kujijenga vema katika misingi ya uongozi, Jakaya Kikwete alijijenga vema katika taasisi hizi za msingi na alipikwa vema.

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni aina ya kiongozi pekee ambaye alihudumu nafasi mbalimbali ndani ya chama na serikali. Safari yake ya uongozi ilianzia ndani ya chama cha TANU. Alikuwa kiongozi wa Vijana wakati wa TANU na baadaye CCM hadi kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi.  Wakati wote katika nafasi zake kwenye chama na serikali, Mh. Kikwete alihimiza maendeleo katika Jimbo lake na watanzania kwa ujumla.

Kimsingi amekuwa chachu ya maendeleo katika kipindi cha urais wake kuanzia mwaka 2005 hadi 2014 ambapo ameshatekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo ambapo mingi imeshakamilika na mingine inategemewa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2015.

2.   HISTORIA YA MAENDELEO

Kimaendeleo, Tanzania ya mwaka 1961 si ya sasa. Tulipopata uhuru mwaka 1961, Tanzania ilikuwa ni nchi changa ambayo haikuwa na mfumo thabiti wenye kuleta maendeleo. Hii ni kutokana na athari tulizozipata wakati wa ukoloni mkongwe (Classical Colonialism) na Ukoloni Mamboleo, Vita ya Kagera na Maanguko ya kimataifa ya Uchumi. Hali hii iliathiri shughuli  za maendeleo kutokufanikiuwa kwa kiwango cha juu. Tanzania ilipitia kipindi kigumu kiuchumi na vita mwaka 1977 mpaka 1979 ambapo ilipelekea athari zaidi kiuchumi hadi miaka ya 1980 ambapo Tanzania ililazimika kukaribia soko huria ili kujenga uchumi. Miaka ya 1990 mpaka miaka ya 2000 Tanzania imesonga mbele kiamendeleo kutokana na juhudi mbali mbali marais ambao wamekuwa wakifanya katika vipindi tofauti vya uongozi wao ambapo Nyerere kutoka 1962 mpaka 1985, Mwinyi kutoka 1985 mpaka 1995, Mkapa kutoka mwaka 1995 mpaka 2005 na kwa sasa tuna Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alianza uongozi kama Rais kuanzia mwaka 2005 mpaka 2015.

3.   MAENDELEO WAKATI WA AWAMU YA NNE CHINI YA UONGOZI WA JAKAYA KIKWETE

Akiwa na dhamira ya kuhakikisha kwamba kila mtanzania anapata fursa sawa katika utumizi wa rasilimali asili na watu zilizopo ili kumjengea uwezo kila mtanzania kufikia kiwango cha maisha bora, Mh. Kikwete alinuia kuboresha maeneo ya msingi yatayowapeleka watanzania katika kilele cha “MAISHA BORA”. Ili kuijenga barabara ya kuelekea katika kilele hiki, awmu ya nne ya serikali yake ilitia mkazo katika maeneo kadhaa kama ifuatavyo:

a)    Kukuza utawala bora.

Mheshimiwa Rais, ni dhahiri kuwa kiwango cha utawala bora katika nchi yetu kimezidi kuimarika siku baada ya siku tena kwa ufanisi mkubwa tangu ulipoingia madarakani. Hilo linathibitika zaidi kwa kuaangalia maeneo mawili makubwa ambayo ni kupunguza urasimu katika shughuli mbalimbali za kiserikali ili kurahishisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi. Mashirika mbalimbali duniani yamekuwa yakitambua mchango wako na kukuwezesha kutunukiwa nishani mbalimbali ambazo hakika ulistahili, kama wasemavyo wahenga “ chanda chema huvikwa pete”

Kutokana na uongozi wako mahiri, Tanzania imepata mafanikio katika nyanja za demokrasia na utawala bora kama ambavyo Mpango wa Afrika wa Kujitathmini katika Utawala Bora (APRM) umebainisha kwamba Tanzania ni kati ya nchi zinazofanya vizuri kwenye eneo la utawala bora.  

 Tanzania imefikia katika kuridhia na kutekeleza mchakato wa Kujitathmini katika Utawala bora kwa nchi za Afrika (APRM) kuwa ni kuwashirikisha wananchi kutoa maoni yao kuhusu hali ya utawala bora nchini na serikali kuruhusu wataalamu wa utawala bora kutoka nchi wanachama kuja nchini kuhakiki mchakato huo. 
Ni ukweli kuwa APRM ni mpango ulioasisiwa Machi 9, mwaka 2013 na wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika (AU)  ambapo Mheshimiwa rais ulikuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha Tanzania inatoa fursa ya kujipima na kujua mwenendo wa serikali na madereva wa utekelezaji (Viongozi wa serikali)
Tanzania kwa sasa ni miongoni mwa nchi 34 kati ya 54 za AU zilizokwishajiunga na mpango huu, ikiwa imejiunga tangu mwaka mwaka 2004. 
Suala la elimu.

Elimu ni nyenzo ya msingi katika jitihada za kujenga uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea na kuwawezesha kiuchumi wananchi. Uchumi wa kisasa unahitaji watenda kazi wenye maarifa yanayohusu kanuni na maarifa ya kumudu vitendea kazi vya aina mbalimbali.
Wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu vilivyopo nchini Tanzania waliongezeka kutoka 55,296 mwaka 2005/2006 hadi 118,000mwaka 2009/2010.Idadi ya vyuo vikuu imeongezeka kutoka vyuo vikuu 23 mwaka 2005 hadi kufikia vyuo 31 mwaka 2010.

Kuweza kujenga chuo kikuu cha Dodoma chenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 40,000 kwa mwaka na kwa sasa kina wanafunzi 17,282

Wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi na kuendelea na elimu ya sekondari wameongezeka kutoka 493,636 hadi 999,070 huku idadi ya wanafunzi wanaogharamiwa na serikali toka familia zenye kipato duni ikiongezeka toka 16,345 hadi 58,843. Ongezeko hili ni kati ya mwaka 2005 hadi mwaka 2009. Pia Uandikishaji katika elimu ya awali umeongezeka kutoka wanafunzi 638,591 hadi wanafunzi 889,363.
Tanzania imeweza kupiga hatua kubwa kwenye utaoji elimu kwa wananchi wake. Kwa kupitia(Mpango Wa Maendeleo wa Elimu ya Msingi) MMEM, MMES na MEMKWA; watoto wengi wa Kitanzania wamepata fursa ya kujiunga na elimu ya msingi na sekondari. Hadi mwaka 2010 zaidi ya watoto milioni 8 (ambao ni zaidi ya 90% ya uandikishaji halisi) wameandikishwa shule za msingi na zaidi ya wanafunzi 1, 638, 699 wako sekondari.
Idadi ya shule na walimu imeongezeka maradufu. Hadi mwaka 2010 shule za sekondari zimeongezeka kutoka shule 937 na kufikia idadi ya 4,2663 mwaka 2010. Walimu nao wameajiriwa kwa idadi kubwa ili kusaidia mchakato wa kuwapatia watoto elimu. Kwa mfano, hadi mwaka 2010 idadi ya walimu wa shule za msingi na sekondari imefikia walimu 206, 3734 kutoka idadi ya walimu 54,869 mwaka 2001. Ongezeko hili limechangiwa na ongezeko kubwa la wanafunzi kwa kuanzia miaka ya 2001 hadi 2010.(tazama jedwali na 1). Hii ni dhahiri kuwa fursa za elimu kwa wote zimeongezeka nchini, na hatuna budi kuipongeza serikali chini ya Rais Jakaya Kikwete na wadau wa elimu kwa jitihada hizo.

Mafanikio katika sekta ya Afya
Mheshimiwa rais, tunapenda kukupongeza kwa kiasi kikubwa kwa jitihada zako katika sekta hii muhimu katika taifa letu. Wote tunafahamu maradhi ni moja kati ya maadui wakubwa ambao wanalisonga taifa letu  toka tupate uhuru.
Ni dhahiri kuwa tangu ulivyoingia madarakani umekuwa ukipambana kwa dhati ili kuhakikisha mapambano juu ya maradhi yanapungua kwa kiasi kikubwa. Wote ni mashahidi kwamba umepigania sana afya ya mama na mtoto kwa lengo moja kuu ambalo lilikuwa ni kupunguza vifo vya kina mama wajawazito pamoja na watoto  kwani hicho kimekuwa ni kilio kikubwa na tatizo kubwa ambalo linazikabili nchi zinazoendelea, kuna msemo usemao ukimsaidia mwamke basi umeokoa jamii nzima, hivyo basi ni dhahiri kuwa kwa nia yako hiyo umefanikiwa kuokoa jamii kubwa sana ya watanzaia wa kizazi kijacho.
Mheshimiwa Rais, umechangia kwa kiasi kikubwa kupambana na ugonjwa wa Malaria ambao umekuwa tishio sio tu Tanzania bali hata Afrika kwa ujumla lakini kwa jitihada zako za dhati kabisa toka moyoni ulikuwa muhamasishaji namba moja katika kupiga vita ugonjwa huu. Ni ukweli usiopingika kampeni mbalimbali kama vile “zinduka”  na zingine ambazo zilibeba dhana ya kuhamasisha jamii kutumia chandarua zimekuwa na mchango mkubwa sana katika jamii yetu.

Mheshimiwa Rais, vilevile umetoa mchango mkubwa sana katika vita dhidi ya ugonjwa hatari kabisa wa ukimwi kwani wakati unaingia madarakani ugonjwa huu ulikuwa ni tishio sana lakini kwa jitihada zako  umefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza maambukizi kama ambavyo takwimu za tume ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) za mwaka 2014 zinatuonesha maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi nchini yamepungua hadi kufikia asilimia 5.1 kwa mwaka 2011/2012  ambapo asilimia 6.2 ni wanawake na asilimia 3.8 ni wanaume.

Mheshimiwa Rais, katika awamu zako mpaka sasa umejitahidi kwa kiasi  kikubwa Katika kuyaendeleza makundi mbali mbali ya kijamii,kwa namna moja ama nyingine, na katika hilo kuna mafanikio ya moja kwa moja ambayo yanonekana kama vile

Wanawake.           
 Hatua ya kurekebisha sheria zinazowabagua na
kuwadhalilisha wanawake katika usawa na maslahi yao imetekelezwa. Sheria ya makosa ya kujamiiana na sheria ya kuwalinda, wajane, zimerekebishwa na Sera ya Hifadhi na Maendeleo ya Wanawake, ziliboreshwa na kusimamiwa kwa kiwango stahiki kwa mfano uanzishwaji wa BENKI YA WANAWAKE pamoja na utoaji wa mikopo mbalimbali mfano mkopo kwa watu wa chini maarufu kama “MABILIONI YA JK”. Pamoja na miradi maalum wa kuinua kipato cha wanawake ili kupunguza ajira mbaya kwa watoto umeanzishwa.

Pia idadi ya wanawake katika nafasi  mbalimbali za juu za uongozi imeongezeka katika kipindi cha 2010-215 kwa mfano nafasi ya spika wa Bunge ambayo kwa sasa anahodhi mwanamke mheshimiwa Anne Makinda.... takwimu zinaonyesha katika kipindi cha uongozi wako nafasi za wanawake bungeni ni...... ambayo ni sawa na asilimia.... ukilinganisha na mwaka....pia hata katika bunge la katiba linaloendelea idadi ya wanawake ni... ..

Walemavu
Ili kulinda na kusimamia haki, usawa na maendeleo ya watu wenye ulemavu, Baraza la Taifa la Maendeleo ya Watu wenye Ulemavu, limeanzishwa chini ya uongozi wa Afisi ya Waziri Kiongozi. Aidha, Sera ya Walemavu imepitishwa na rasimu ya awali ya Sheria ya Walemavu imekamilika.
Hatua za kuelimisha jamii juu ya masuala mbali mbali ya kuwaendeleza watu wenye ulemavu, zimetekelezwa. Jumla ya watu 219 wenye ulemavu wamepatiwa mafunzo ya uendeshaji wa biashara ndogo ndogo Unguja na Pemba pamoja na kupatiwa mkopo wa kujiendeleza. Watu 193 wenye ulemavu wa kutosikia (viziwi)
wamepatiwa mafunzo ya lugha ya ishara.

Miundo mbinu
Kipindi cha miaka kumi iliyopita cha 2000 – 2010 tumeshuhudia kuwepo kwa
ujenzi mkubwa wa miundombinu ya barabara, viwanja vya ndege na madaraja nchini. Miradi yote ya ujenzi ambayo haikukamilishwa kati ya 2000 – 2005 imekamilishwa kati ya 2005 – 2010 na kuanzishwa ujenzi wa miradi mipya kitakwimu, ujenzi wa miradi 15 kwa kiwango cha lami yenye jumla ya urefu wa Km. 1,398.6 imekamilishwa katika kipindi cha 2005 - 2010. Aidha, ujenzi ambao unaendelea ni wa miradi 29 ya barabara zenye jumla ya Km. 2,536.4 na wakati huo huo miradi 7 ya barabara yenye jumla ya Km. 1,562 inaendelea kufanyiwa upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi. Hiki ni kielelezo dhahiri cha mafanikio makubwa ambayo yameiweka nchi yetu katika chati ya kuwa na miundombinu ya kisasa ya barabara.  Mwelekeo wa Sera za  serikali yako  katika miaka ya 2010 hadi 2020 umeainisha jukumu kubwa la nchi yetu katika kipindi hiki ni kutekeleza lengo la Dira 2025 la kuleta mapinduzi ya uchumi yatakayoitoa nchi kutoka kwenye dimbwi la uchumi ulio nyuma na tegemezi na kuiingiza katika mkondo wa uchumi wa kisasa wa taifa linalojitegemea.
Dhana ya Kujenga Uchumi wa Kisasa inalenga katika modenaizesheni ya uchumi.
Modenaizesheni kimsingi ni kuongeza maarifa na matumizi ya sayansi na teknolojia
katika sekta za uzalishaji. Modenaizesheni ya uchumi inalenga katika kuongeza
uzalishaji, ufanisi na tija katika uchumi hususan katika kilimo, ufugaji, uvuvi na
viwanda.

Mapinduzi ya Kilimo
Kilimo ndio msingi wa uchumi wa kisasa na njia sahihi ya kuutokomeza
umasikini.
Mheshimiwa rais umekuwa muumini wa dhati kwamba kilimo cha kisasa
kinachotumia Kanuni na zana bora za kilimo ndio ufunguo wa maendeleo ya
uchumi wa nchi yetu. Kilimo cha kisasa kina uwezo wa kutoa mazao mengi zaidi
kutoka kila ekari iliyolimwa. Kwa nchi yetu, ziada hiyo ya mazao ina faida kubwa
zifuatazo:-
(a) Kuipatia kila familia, kijiji na Taifa chakula cha kutosha ili kukomesha njaa.
(b) Kulipatia Taifa mavuno mengi ya kuuza ili kupata fedha za kigeni kwa ajili
ya maendeleo ya nchi.
(c) Ziada ya mazao huunda mazingira muafaka ya kuanzishwa viwanda vya
usindikaji na utengenezaji wa bidhaa za viwandani.
(d) Familia yenye ziada ya mazao huutokomeza umaskini kwa kuuza ziada
hiyo kwenye soko na kupata fedha za kujiletea maendeleo.
32. Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ya utekelezaji wa Ilani ya mwaka 2005-
2010, Serikali zetu zilichukua hatua kubwa katika kukipatia kilimo mwelekeo wa
kisasa ili kiondokane na zana duni, mashamba madogo, kutozingatia kanuni bora
za kilimo na kuridhika na mavuno ya kujikimu.

Mheshimiwa Rais, kwa heshima na taadhima tunapenda kukupongeza kwa dhati kwa kuanzisha mchakato wa Katiba mpya licha ya changamoto zilizojitokeza katika mchakato huo. Sote tunatambua nia yako ya dhati kuhakikisha taifa letu linapata katiba mpya kabla hujamaliza awamu yako ya pili ya uongozi hapo mwakani. Tunakusihi mchakato huu usiwe chanzo cha machafuko nchini mwetu bali maridhiano ya kisiasa yawe ndio msingi mkuu wa kupatikana kwa katiba itakayolivusha taifa letu kwa miaka mingi ijayo. Mwisho tunakutakia safari njema na mafanikio tele katika kutekeleza majukumu yako.


4.   CHANGAMOTO

a)    Kushuka kwa thamani ya shilingi

Shilingi ya Tanzania imekuwa haijatengamaa kwa vipindi tofauti tofauti ukilinganisha na Dola ya Kimarekani. Hali hii haijawa chachu katika juhudi za kimaendeleo zinazofanyika. Katika suala la kushuka kwa thamani ya shilingi, Serikali inatakiwa kujenga uchumi imara uliojengeka kwenye shilingi iliyoimara ukilinganisha na Dola ya Kimarekani

b)   Bajeti isiyotosheleza mahitaji

Bajeti ya Tanzania imekua isiyojitosheleza hasa kwa kuwa ni bajeti  tegemezi. hii imesasababisha mambo mengi kukwama.  wahisani wengi wamekua hawaleti pesa kwa wakati au kuleta fedha kwa masharti magumu yanaitesa nchi. Vyanzo vingi vya mapato vimekua visivyotosheleza na hivyo kupelekea bajeti ya maendeleo kuwa finyu ukilinganisha na mahitaji.       Katika suala hili  tunaishauri, Serikali ibuni vyanzo vipya na vya mbadala vya mapato ili kukusanya fedha ya kutosha itakayotoshereza mahitaji ya kibajeti

c)    Rushwa na ufisadi,

hili ni tatizo na tishio katika maedeleo ya Tanzania, viongozi wengi katika sekta mbalimbali Serikalini na hata sekta binafsi wamekuwa si waaminifu tena. Wamekuwa wakidai rushwa za aina tofauti au kufanya ufisadi, ubadhirfu wa fedha na hivyo kuathiri kwa kiasi kikubwa kasi ya maendeleo katika sekta mbalimbali.

d)    Kushuka kwa uzalendo

Watanzania wa sasa si wa zamani. Zamani kulikuwa na misingi ya kimaadili na mafunzo iliyopelekea watanzania wengi kuipenda nchi yao na hivyo kupelekea kuwa wazalendo. Hali si hivyo tena kwa sasa, hii ni kutokana na kuibuka kwa changamoto mbalimbali za sayansi na teknolojia hivyo kumepelekea watu kuwa wabinafsi zaidi kuliko kujali masuala yanayohusu watanzania kwa jumla.

5.   HITIMISHO

          Mwisho kabisa mheshimiwa Rais, tunapenda kutoa pongezi zetu za dhati kwa kutunukiwa nishani mbalimbali kutoka sehemu tofauti duniani ikiwa ni ishara ya wao kutambua mchango wake baadhi ya nishani hizo ni kama Nishani Ubora wa Lulu ya Afrika (Bwana tukufu) Julai 2007 Nishani ya Hilali Kijani ya Komori Machi 2009,Nishani ya Abdulaziz Al Saud ,Aprili 2009,Nishani ya Ubora  Novemba 2009 ,Nishani ya Oman , Oktoba 2012 pamoja na tuzo za hivi karibuni za Tuzo la Nyota wa Demokrasia Afrika  2014 – Icon of Democracy Award Winner for 2014 in Africa
         Wewe ni kioo kwetu kama vijana na wapiganaji wengine wote, tutakufanya mwenye tabasamu siku zote kwa kuishi uvumilivu wako wa kisiasa na kiumbe kinachopenda mwafaka pale maslahiya kitaifa yanapotamalaki.

Wenu Mtiifu,
 Loveness Mamuya – Kada Mzalendo CCM Marekani

No comments: