Saturday, August 2, 2014

Profesa Elisante Ole Gabriel mgeni Rasmi katika mahafali ya Shule ya Awali ya Sunrise jijini Dar

Lango kuu la kuingilia katika Shule ya Msingi na Awali ya Sunrise iliyopo jijini Dar es Salaam likiwa na maandishi ya kukaribisha wageni katika mahafali ya Saba ya Shule hiyo yaliyofanika jana.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akipokea zawadi ya maua kutoka kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya Saba ya wahitimu wa Darasa la Saba jana.
Mwanafunzi anayehitimu Darasa la Saba katika Shule ya Msingi na Awali Sunrise Bw. Mark Ngalo akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wenzake wakati wa mahafali yao yaliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.Aliyemshikia kipaza sauti ni Lulu Benson.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na M,ichezo Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza na wazazi na wanafunzi wakati wa mahafali ya wahitimu wa Darasa la Saba wa Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam jana alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na M,ichezo Profesa Elisante Ole Gabriel akimkabidhi Cheti mmoja wa wahitimu wa Darasa la Saba katika Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya Saba ya Shule hiyo yalifanyka jana jijini Dar es Salaam. Katika ni Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Onesmo Vitalis.
Kikundi cha Skauti cha Shule ya Msingi na Awali Sunrise wakitoheshi mbele ya mgeni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel (hayupo pichana) alipokuwa mgeni rasmi katika mahafa ya saba kwa wahitimu wa Darasa la Saba katika shule hiyo jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi na Awali ya Sunrise wakifurahia kwa michezo wa sanamu wakati mahafali ya darasa la Saba jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wahitimu wa Darasa la Saba wa Shule ya Msingi na Awali Sunrise ya jijini Dar es Salaam wakiwa wenye nyuso za furaha wakati wa mahafali yao jana jijini Dar es Salaam.



No comments: