Monday, August 25, 2014

DKT. SHEIN AWAAPISHA MAWAZIRI WAPYA IKULU ZANZIBAR LEO

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Dk.Sira Ubwa Mamboya kuwa Waziri wa Kilimo na Maliasili katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar kabla Dk.Sira alikuwa Naibu Waziri wa Afya.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Juma Duni Haji kuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar kabla alikuwa Waziri wa Afya.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Rashid Seif Suleiman kuwa Waziri wa Afya,awali alikuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano hafla ya kiapo imefanyika katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Mahmoud Thabit Kombo kuwa Naibu Waziri wa Afya, hafla ya kiapo imefanyika katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Meja mstaafu Juma Kassim Tindwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja,katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar kabla alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw.Omar Khamis Othman kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Mwanajuma Majid Abdulla kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo ,kabla alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Pemba.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw.Ayoub Mohamed Mahmoud kuwa Mkuu wa Wilaya Magharibi leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,awali alikua Afisa Tawala katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mjini magharibi Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bibi Hanuna Masoud Ibrahim kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chake chake Pemba leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar. (Picha na Ramadhan Othman Ikulu.)

No comments: