Tuesday, July 29, 2014

UGAIDI HAUNA UHUSIANO NA DINI ASEMA SHEIKH ATAKA VIONGOZI WA DINI ZOTE KUKUTANA NA SERIKALI KUTAFUTA MFADHILI WA UGAIDI NCHINI

kaimu sheikh wa  mkoa  wa  Iringa  Abubakar Chalamila
Waumini  wa  dini ya kiislamu mjini  Iringa  wakiwa katika ibada ya idd uwanja wa Samora  leo
Ibada ya  idd ikiendelea katika uwanja wa Samora mjini Iringa  leo
Waumini wa dini ya  kiislam  Manispaa ya  Iringa  wakiswali  pamoja  ibada ya  Idd leo
Waumini wa dini ya Kiislam Iringa  wakiwa katika ibada 
Mwenyekiti wa CCM Iringa mjini Abed Kiponza wa tatu  kushoto akishiriki ibada ya Idd
Mwenyekiti wa CCM Iringa mjini Abed  Kiponza  akiwa na Sheikh Wanguvu  kulia mara baada ya  ibada ya Idd
Aliyekuwa  mwenyekiti wa UVCCM Iringa mjini Ibrahim Ngwada  akiwa na mmoja kati ya  watoto  walioshiriki ibada ya  Idd wakipongezana kwa kumalizika kwa mwezi mtukufu
Furaha ya  Idd Iringa
Wazee maarufu na makada  wa  CCM ambao ni waumini wa dini ya Kiislam  wakipiga picha ya pamoja na mwenyekiti wa CCM Iringa mjini Abed Kiponza  kulia  wa pili  kulia ni Mr  Mbata
katibu mkuu wa watuma  salam mkoa wa Iringa Mood Mambo  akifurahia  jambo baada ya  kumalizika kwa swala ya Idd  leo

Wadau  maarufu wa matukiodaioma Iringa katika picha ya pamoja
Mzee wa matukiodaima  wa pili  kulia akiwa na wadau wake
 Na MatukiodaimaBlog
WAKATI  matukio ya  uvurugaji  wa amani yanayohusishwa na  vitendo  vya ugaidi   yakiendelea  kuota  mbawa  nchini , kaimu  sheikh wa  mkoa  wa  Iringa  Abubakar Chalamila amewataka  waislamu  na  viongozi  wa  dini  zote nchini  kuendelea  kuliombea  Taifa   huku akidai kuwa matukio  hayo ya ugaidi  yanayoendelea  hayana mahusiano  na dini  yoyote isipo kuwa  wapo baadhi ya  wana siasa  wanatumia mwanya  huo  kwa  matakwa  binafsi ya kuligawa  Taifa.

Akizungumza  jana  mara  baada ya  swala  ya  Idd  iliyofanyika  katika  uwanja  wa  Samoraka  Sheikh Chalamila  alisema siku  zote  toka  nchi  inapata  uhuru  wake mwaka 1961 dini  ya  Kiislam  na  kikristo  zilikuwepo na  hakukuwa na matukio ya  kigaidi  kama yanayojitokeza  sasa  kwa maparoko  na  masheikh  kuvamiwa  na kumwangiwa  tindikali na  hata baadhi ya maeneo  kutokea milipuko ya mabomo kama mkoani  Arusha na  Zanzibar .

Kwani  alisema  iwapo  kungekuwa na vita  za  kidini kama zilizo nchi  inyinge  duniani  kweli  akiwa kama  kiongozi  wa  dini  angekuwa ni  mtu wa kwanza kuamini  kuwa  matukio  hayo ya  kigaidi  yanayotokea  yanamahusiano ya karibu  na  dini  ila uongozi  wa nchi  yetu  toka hayati  baba  wa taifa  Mwalimu  Julius Nyerere hadi Rais wetu  Jakaya  Kikwete wameendelea  kuliunganisha  Taifa na  kuwa  pamoja bila  kuwepo kwa  misuguano ya  kidini .

" Sasa  kama  watanzania  tu  wamoja  kwa muislamu na Mkristo  kukaa pamoja  kama  ilivyo  hivi  iweje ugaidi  uwepo  ......ugaidi kati ya  dini na  dini  hutokea pale  penye tofauti  na misuguano  ila  katika Taifa  letu hakuna misuguano baina ya waislam na  wakristo  kila mmoja ana abudu kwa  uhuru  ....ila  wapo  watu  siwezi kusema  moja kwa moja kama ni  wana siasa ama vipi  ila  wapo  wanaotaka  kutugawa kwa misingi ya dini ili  kufanikisha mambo yao ya  kisiasa ama  ya  kiuchumi "

Hivyo  alisema  ili  kuweza  kubaini mbaya  wetu anayesababisha machafuko nchini ni  vema  viongozi  wa  dini  zote na  serikali  kukaa meza  moja  ili  kutafuta  mchawi  wetu kabla  ya kumwacha aendelee  kufanya  hivyo  kwa  iwapo ufumbuzi hautapatikana na mtu  huyo ama  watu hao  wakifanikiwa  kutugawa  basi  ni  wazi  nchi  itaingia katika machafuko mabaya  zaidi.

" Nafasi  bado  tunayo nawaomba  viongozi wa  serikali  watuite  viongozi wa  dini  ili  tukae kwani watu hawa  wanataka  kutuvuruga  kwa  misingi ya  kisiasa ama  udini .."

Akielezea  kuhusu   mwenendo  wa Taifa  alisema  kuwa hali si nzuri  kutokana  na  watu kukwepa  maadili ya Taifa letu  na  ndio  sababu ya majanga  mbali mbali  yanaendelea  kujitokeza na  hivyo kutaka  watanzania  kurejea katika maadili  ikiwa ni  pamoja na viongozi wa  dini  kuzidi kuhubiri amani na  kuliombea Taifa.

Katika  hatua  nyingine  Sheikh  Chalamila  alisema  kuwa pamoja na  kuwepo kwa madai kutoka  kwa baadhi ya  watu  kuwa  waislamu  si  wamoja  kutokana na  kutofautiana  siku ya kuswali  Idd  ila  ukweli  ni  kuwa waislam  ni  wamoja na  wameshikamana  isipo kuwa  tofauti ya kuanza  kufungua  inatokana na matawi  katika  dini  hiyo kama zilizodini  nyingine  hivyo  si jambo  la  kuwaona kama  hawapo  pamoja

No comments: