Wednesday, June 4, 2014

PANONE FC YAPOKELEWA KISHUJAA MKOANI KILIMANJARO

Msafara wa magari ukiongozwa na mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Kilimanjaro Goodluck Mushi wakipita katika maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi mara baada ya kuwasili wakitokea jijini Mbeya ambako timu hiyo imefanikiwa kupanda ligi daraja la kwanza.
Wachezaji wakishuka katika basi la Hood baada ya kuwasili mjini Moshi.
Furaha ilikuwa kubwa katika eneo hilo mara baada ya timu kuwasili.
Kama vile viongozi wa timu hawaamini kuwa wako katika ardhi ya nyumbani Moshi .
Wachezaji wengine walikuja kupokelewa na wazazi wao.
Baadhi ya wachezaji wakiwa nje ya jengo la Posta katikati ya mji wa Moshi walipoteremka mara baada ya kurejea wakitokea mkoani Mbeya.
Katibu  wa chama cha soka mkoa wa Kilimanjaro (KRFA)Mohamed Musa(mwenye suti) akiteta na viongozi wengine waliofika katika mapokezi ya timu hiyo akiwemo mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Hai,Harold Kifunda(mwenye begi)
Meneja wa kampuni ya Panone Ltd kanda ya kaskazini Gido Marandu akiwa na mwandishi wa habari za Michezo wa kituo cha radio cha Moshi fm wakibadilishana mawazo katika hafla ya chakula cha mchana katika mgahawa wa Fresh Coach muda mfupi baada ya mapokezi.
Makocha wa timu ya Panone fc ,Jumanne Ntambi na Atuga Manyundo wakiteta jambo wakati wa chakula cha mchana kwa timu hiyo katika Mgahawa wa Fresh Coach.
Wachezaji wa klabu ya Panone fc ya mkoani Kilimanjaro wakiwa katikaMgahawa wa Fresh Coach wakipata chakula cha mchana kilichoandaliwa na uongozi wa Kampuni ya Panone Ltd.
Picha na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii, Moshi

No comments: