Wednesday, April 9, 2014

HATIMAYE WASHINDI WATATU WA MASHINDANO YA KUSAKA VIPAJI VYA UIGIZAJI (TANZANIA MOVIE TALENTS) KWA KANDA YA ZIWA WAPATIKANA LEO JIJINI MWANZA

.
Washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya 15 bora wakiwa mbele ya majaji tayari kwa kuchaguliwa washiriki watano bora.
Hawa ndio washiriki walioingia tano bora
Emiliana Fidelis akiwa amesimama mbele ya meza ya majaji mara baada ya majaji kufurahishwa na kuvutiwa na Kipaji chake, Emiliana ni mmoja kati ya waliotakiwa kuwa mshindi wa Kanda ya ziwa ila kwa bahati mbaya Umri wake ndio ulikuwa kikwazo.
Jaji Yvonne Cherry akimkabidhi zawadi ya shilingi laki Moja Mshiriki Emiliana Fidelis mara baada ya kuvutiwa na Kipaji chake huku akiwa mshiriki pekee mwenye umri mdogo kuliko wote kwenye mashindano ya Kusaka Vipaji vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents.
Jaji Mkuu wa Mashindano ya Kusaka vipaji vya kuigiza Tanzania yajulikanayo kama Tanzania Movie Talents, Roy Sarungi akimkabidhi zawadi mmoja wa Washindi watatu wa mashindano hayo mara baada ya kutangazwa washindi.
Jaji Single Mtambalike akimpongeza mmoja wa washiriki aliyefanikiwa kuibuka kidedea katika Mashindano ya Tanzania Movie Talents.
Mshiriki Crensenciah Herman akilia kwa furaha mara baada ya Kutajwa kuwa mmoja kati ya washindi katika shindano la kusaka vipaji vya uigizaji Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents lilomalizika Leo Mkoani Mwanza
Majaji wakiwa katika picha ya Pamoja na washindi watatu wa Kanda ya Ziwa Mkoani Mwanza mara baada ya Kuwatangaza na kuwakabidhi washindi zawadi zao.Picha na Josephat Lukaza wa Proin Promotions Limited - Mwanza

No comments: