Saturday, March 1, 2014

YANGA YAITANDIKA AL AHLY BAO 1 - 0 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR LEO

 Kikosi cha Yanga 
 Kikosi cha Al Ahly
 Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Mrisho Ngassa akiondoka na mpira huku Beki wa Timu ya Al Ahly ya Misri akitafuta namna ya kumzuia katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
 Kiungo mchezeshaji wa Yanga,Haroun Niyonzima akitafuta namna ya kuwatoka mabeki wa Timu ya Al Ahly ya Misri katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
 Kiungo mchezeshaji wa Yanga,Haroun Niyonzima akizuiwa na Beki wa Timu ya Al Ahly ya Misri,Ramy Abdel Aziz katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
Kipa wa timu ya Al Ahly ya Misri,Sherif Ekramy Ahmed akida moja ya hatari iliyokuwa ikielekeshwa langoni kwake na Mshambuliaji wa Yanga,Hamis Kiiza.
 Heka heka ya kuwania mpira wa Kichwa.
 Mshambuliaji Machachari wa timu ya Yanga,Emmanuel Okwi akiwachachafya mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri katika mchezo wao uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wa kuwania tiketi ya kusheza 16 bora ya Klabu Bingwa Barani Afrika.katika mchezo huo,Yanga imeifunga timu ya Al Ahly bao 1 - 0. 
 Emmanuel Okwi wa Yanga akichezewa faulo na mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri.
 Heka heka langoni mwa timu ya Al Ahly.
Mshambuliaji Emmanuel Okwi wa Yanga leo ndio alikuwa mwiba kwa timu ya Al Ahly,maana alikuwa akikabwa na Mabeki wawili wawili........
 Kipa wa timu ya Al Ahly ya Misri,Sherif Ekramy Ahmed akiruka mithili ya nyani wakati akiokoa moja ya hatari zilizokuwa zikielekezwa langoni kwake.
 Okwi anatafuta namna ya kuchia shuti.
 Mshambuliaji wa Yanga,Didier Kavumbagu akiwania mpira na Mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri.
 Ulinzi maridhawa kabisa ulitawala Uwanjani hapa.
 Ilikuwa ni nyomi la hatari.
Wachezajiwa timu ya Yanga wakishangilia ushindi wao sambamba na Mashabiki wao lukuki waliofurika uwanjani hapa.

Mfungaji wa bao pekee la Yanga,Nadir Haroub akirejea uwanjani baada ya kutoka kushangilia pamoja na washabiki wao.
 Benchi la ufundi la Al Ahly ya Misri.
 Benchi la Yanga.
 Mashabiki wa Al Ahly wakishangiliwa mwanzo mwisho,wakisaidiwa na Mashabiki wa timu ya Simba. 
 Okwiiiiiiii.......
Kocha wa Al Ahly akihaha kutoa maelekezo kwa Wachezaji wake. 
 Mabeki wa timu ya Yanga,Nadir Haroub pamoja na Kelvin Yondani wakiwa wamejipanga vyema kuuzuia mpira wa Mshambuliaji wa timu ya Al Ahly,Moussa Yedan.
 "Poa tu mwana,hii ni fea pleii tuuuuu......" 
 Ni shangwe tupu kwa Mashabiki wa timu ya Yanga uwanjani hapa hii leo. 
Mashabiki wa timu ya Al Ahly wakifungasha virago vyao baada ya kulala kwa bao 1 - 0.
 Kocha wa Yanga akisema na wachezaji wake mara baada ya kipenga cha mwisho kulia.
 Kufungwa kubaya jamaniiiiii....
 Mara baada ya Yanga kupata Goli la kwanza na la pekee,Mashabiki wa Simba walianza tena kunyoa viti na kuwarushia mashabiki wa timu ya Yanga waliokuwa wakishangilia ushindi wao huo. 
 Wazee wa feva wakiwatuliza washabiki hapo wa Simba.
Cheki mapengo ya kung'olewa kwa viti uwanjani hapa.Hali hii ni nani anatakiwa kuidhibiti???

2 comments:

Unknown said...

hiyp ndio dar yang afr bwana si mchezo

Unknown said...

hiyo ndio yanga bwana si mchezo