Tuesday, March 4, 2014

KUZIBA KWA MITARO KWAPELEKEA MAJI KUJAA KWENYE STENDI YA MWENGE,JIJINI DAR

 Hii ni sehemu ya maduka ambayo kwa mbele ya hayo maduka maji yamejaa kutokana na kuziba kwa mitaro ya eneo la stendi ya daladala ya Mwenge jijini Dar es salaam,hali hii imekuja kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha hivi sasa hapa jijini.
 Sehemu hii kuna mtaro wa maji lakini kutokana na kuziba kwake imekuwa kero kwa wafanyabiashara na watu wanaotumia stendi ya Mwenge kwani mitaro hiyo imeziba na kupelekea maji kujaa na kuingia barabarani hata madukani.
 Unaweza kusema ni mto lakini kumbe ni maji ya mvua yaliyotuhama kutokana na mitaro kuziba
 Kutokana na kuziba kwa mitaro hiyo maji yanaingia mpaka kwenye barabara ya Bagamoyo inayopita karibu na kituo hicho cha Mwenge.

No comments: