Thursday, February 27, 2014

Mhe. Membe alipokutana na Makamu wa Rais wa China mjini Beijing

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao alipokutana nae kwa mazungumzo kwenye Jumba la Mikutano la Kitaifa la China maarufu kama People's Great Hall mjini Beijing, China. Mhe. Membe yupo nchini humo kwa ziara ya kikazi ya siku tano kuanzia tarehe 24 hadi 28 Februari, 2014.
Mhe. Membe na Mhe. Yuanchao wakiendelea na mazungumzo.
Mhe. Membe akiagana na Mhe. Yuanchao mara baada ya mazungumzo yao.

....Mhe. Membe alipokutana na Makamu Waziri wa Usalama wa Raia wa China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwa katika mazungumzo na Mhe. Wang Hanning, Makamu Waziri wa Usalama wa Raia wa Jamhuri ya Watu wa China alipokutana nae mjini Beijing wakati wa ziara ya kikazi ya Mhe. Membe nchini China tarehe 26 Februari, 2014.
Mhe. Membe akiendelea na mazungumzo na Mhe. Hanning huku Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Abdulrahman Shimbo (kulia kwa Mhe. Membe) na wajumbe waliofuatana na Mhe. Hanning wakisikiliza.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Mhe. Li Jinzao, Makamu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China kabla ya kufanya mazungumzo rasmi na Waziri huyo wakati wa ziara yake nchini China.
Mhe. Membe (kulia) na Ujumbe wake wakiwa kwenye mkutano wa pamoja na Mhe. Jinzao (kushoto) na ujumbe wake.

No comments: