Thursday, February 13, 2014

MAKAMU WA RAIS,DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA UWEKEZAJI KANDA YA ZIWA,JIJINI MWANZA LEO

  Mgeni Rasmi katika Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohammed Gharib Bilal akitoa hotuba yake wakati wa Ufunguzi wa Kongamano hilo,uliofanyika mapema leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika,Jijini Mwanza.
 Mwenyekiti wa Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,Mh. George Kahama akitoa hotuba yake wakati wa Ufunguzi wa Kongamano hilo,uliofanyika mapema leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika,Jijini Mwanza.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Mh. Evarist Ndikilo ambaye ndie Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,akizungumza na washiriki wa Kongamano hilo (hawapo pichani) wakati ufunguzi wake uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Malaika,Jijini Mwanza.
 Waziri wa Viwanda na Biashara,Mh. Abdallah Kigoda akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi kuja kuzungumza na Washiriki wa Kongamano hilo,jijini Mwanza leo.
Balozi wa Afrika ya Kusini nchini Tanzania,Mh. Thamduycse Chilliza (katikati) akifatilia Kongamano hilo sambamba na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC),Julieth Kairuki (kushoto).Kulia ni Msaidizi wa Balozi wa Afrika Kusini,Terry Govender.
Waheshimiwa Mawaziri wakishiriki pamoja na Wajumbe wa Kongamano hilo,kuimba wimbo wa Taifa.
Baadhi ya waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya.
Wadau wa Bodi ya Utalii.
Washiriki mbali mbali wa Kongamano hilo.
Watumishi wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Wadau wakifatilia kwa umakini Kongamano hilo.



Picha ya pamoja na Waheshimiwa Mawaziri na Wakuu wa Mikoa.
Picha ya Pamoja na Watumishi wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Picha ya Pamoja na Baadhi ya wawekezaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini,Julieth Kairuki (mwenye fulana nyeupe) akionyesha kitu kwa Makamu wa Rais,Dkt. Mohammed Gharib Bilal wakati alipokuwa anakenda kutembelea Mabanda ya wawekezaji mbali mbali wanaoshiriki kwenye Kongamano la Uwekezaji,jijini Mwanza.
Makamu wa Rais,Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa Kituo cha Uwekezaji Kanda ya Ziwa,Fanuel Lukwaro (wa pili kulia) wakati alipotembelea Banda la Kituo hicho kwenye Maonyesho ya Kongamano la Uwekezaji yanayoendelea kufanyika jijini Mwanza hivi sasa.Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Mh. Everist Ndikilo na kulia kwa Makamu wa Rais ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini,Julieth Kairuki.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini,Julieth Kairuki akimueleza jambo Makamu wa Rais,Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Makamu wa Rais,Dkt. Mohammed Gharib Bilal akipatiwa maelezo ya Kibenki toka kwa Meneja wa Akaunti wa Benki ya EcoBank,Saleh Said wakati alipotembelea banda hilo.
Makamu wa Rais akisikiliza maelezo katika Banda la wawekezaji wa VicFish na KukuPoa.
Makamu wa Rais katika Banda la PPF.

























No comments: