Monday, January 6, 2014

ZIARA YA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA ZANZIBAR MAALIM SEIF KTK BANDA LA TASAF

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na Afisa Mawasiliano wa TASAF Zablon Bugingo 
Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akitia saini kitabu cha wageni alipotembelea banda la TASAF
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisikilkiza  maelezo kuhusu  faida na matumizi ya asali ya masega kutoka kwa  Khamis Suleiman Masoud wa kikundi cha JUKUNUM Cooperative cha Vitongoji Kibokoni Pemba 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akipewa maelezo ya namna ya kutengeneza lulu toka kwenye gamba la Chaza Bahari na Mwajuma Haji Sharif (wa kwanza kulia mwenye kofia) toka kikundi cha Tujikomboe Co-operative Makombeni Pemba . Wa pili kulia ni Nasra Yusuf Yakuob wa kikundi cha Mwendapole Co-operative Mangapwani Unguja  
Lulu ikionekana (vidoti) ikiwa imeganda katika gamba la Chaza Bahari kama vilivyokuwa vikioneshwa na washiriki toka Tujikomboe Co-Operative Makombeni Pemba katika Banda la TASAF 
Chaza Bahari za ukubwa mbalimbali zikiwa na Lulu iliyotengenezwa kwa mtindo wa aina yake zikiwa katika banda la TASAF, bidhaa hizi zinawavutia watu wengi ambao walitembelea banda la TASAF 
Baadhi ya bidhaa zitokanazo na gamba la Chaza Bahari na vile vitokanazo na Lulu iliyooteshwa kwa taaluma maalum kwenye gamba la Chaza Bahari vikiwa kwenye meza ya maonesho katika banda la TASAF (viwili vya Kushoto ni heleni na kulia ni Pete)
Pete iliyotengenezwa kutokana na Chaza Bahari ikiwa imevaliwa katika kidole cha mkono wa mtazamaji aliyetembelea banda la TASAF
Mratibu Msaidizi wa TASAF Unguja  Ali Kassim akikabidhi mfuko wenye makabrasha mbali mbali ya TASAF kwa Makamu wa Kwanza wa Rais Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad alipotembelea banda la TASAF
SEhemu ya wananchi mbali mbali waliofika kwenye banda la TASAF kupata habari na makabrasha mbali mbali kuhusu TASAF wakati wa maonesho miaka 50  ya Mapinduzi ya  Zanzibar 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akipokelewa na Mratibu msaidizi wa TASAF Ali Kassim katika banda la TASAF

No comments: