Sunday, December 1, 2013

Ziara ya Kinana Wilayani Chunya, mkoa wa Mbeya

 Katibu wa NEC, Itikasi na Uenezi Nape Nnauye akiruka kwenye moja ya maeneo yanaotengenezwa kwenye barabara hiyo, inayopita kwenye safu ya milima, wakati wa ukaguzi wa barabara hiyo inayotengenezwa na kampuni ya kichina ya CCCC. Nyuma yake ni Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana mbaye pia aliruka
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (wapili kulia) akikagua ujenzi wa barabara ya lami ya eneo la kilometa 30 kutoka Mbeya hadi Chunya, wakati msafara wake ulipopita katika barabara hiyo ukienda Chunya, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi na kujaduiliana nao njia za kuzitatua mkoani Mbeya, Nov 30, 2013. Kulia ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na watatu ni Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro na Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro anaofuatana nao kwenye ziara hiyo.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipandisha bendera kuzindua shina la wajasiriamali wa CCM, katika kituo cha mabasi cha mjini Chunya, akiwa katika ziara kukagua utekelezaji wa ilani ya chama, kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia sahihi ya kuzitatua, mkoani Mbeya, Nov 30, 2013.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi baada ya kuzindua shina la wajasiriamali wa CCM, katika kituo cha mabasi cha mjini Chunya, akiwa katika ziara kukagua utekelezaji wa ilani ya chama, kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia sahihi ya kuzitatua, mkoani Mbeya, Nov 30, 2013.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimsikiliza Kijana, Frank Mwapololo, ambaye ni mmoja wa wachimbaji wadogo katika machimbo ya mafunzo kwa ajili ya wachimbaji wadogo, yaliyopo Chunya, alipozungumza na wajasiriamali wa mradi huo, Nov 30, 2013, akiwa katika ziara kukagua utekelezaji wa ilani ya chama, kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia sahihi ya kuzitatua, mkoani Mbeya.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye (wapili kulia) akimrekebishia sawasawa vazi, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, baada ya wazee wa Kata ya Lupa, wilayani Chunya, kumvalisha vazi la wazee wa Kata hiyo, akiwa katika ziara kukagua utekelezaji wa ilani ya chama, kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia sahihi ya kuzitatua, mkoani Mbeya, Nov 30, 2013.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikabidhi mashine isiyotumia umeme, ya kufyatulia matofali, kwa kikundi cha wajasiamali, wakati wa mkutano wa hadhara aliofanya Nov 30, 2013, katika Kata ya Lupa, wilayani Chunya, akiwa katika ziara kukagua utekelezaji wa ilani ya chama, kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia sahihi ya kuzitatua, mkoani Mbeya, Nov 30, 2013. Wengine ni Mkuu wa mkoa huo, Abbas Kandoro na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Picha zote na Bashir Nkoromo

1 comment:

Anonymous said...

kazi nzuri bw. kinana