Wednesday, December 25, 2013

WAKAZI WA MTWARA WAJITOKEZA KWA WINGI KUFANYA USAFI WA MJI WAO

MKUU wa wilaya ya Mtwara,Willman Ndile amewahimiza wakazi wa Manspaa ya Mtwara Mikindani kuendelea kujitokeza kwa wingi kushiriki katika kampeni ya kufanya usafi wa mazingira ya mji aliyoianzisha ili kuuweka mji uo katika hali ya usafi.

Ndile aliyasema hayo alipokuwa akiongea mara baada ya kukamilika kwa zoezi la usafi jana katika eneo la Bima mjini hapa ambapo alisema, ni jambo jema wananchi wanapojitokeza kushiriki katika shughuli za kijamii kuoneshwa namna ambavyo serikali inajali mchango wao licha ya kuwa ni wajibu wao kufanya hivyo.

Alisema katika siku ya kwanza ya kampeni hiyo wananchi wengi wamejitokeza hali inayomtia hamasa zaidi kuendeleza kampeni hiyo na sasa itakuwa ikifanyika kila siku ya mwisho wa wiki na kuwataka viongozi wa mitaa na kata kuweka mikakati na mipango mizuriya kutekeleza zoezi hilo katika maeneo yao.

Hatua hiyo ya Mkuu huyo wa wilaya kuanzisha kampeni hiyo inatokana na kukithiri wa uchafu kwenye maeneo ya Manspaa ya Mtwara Mikindani huku mamlaka husika zikitupiana lawama kati yao na wananchi na taasisi mbalimbali kuwa ndio wenye jukumu la kufanya usafi hali inayofanya kuwapo kwa vichaka katikati ya mjini na marundo makubwa ya takataka katika makazi ya watu.

Katika kampeni hizo watu mbalimbali walijitokeza wakiwemo wakazi wa manspaa, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, watendaji wa serikali na waandishi wa habari ambapo walishiriki kufanya usafi katika eneo ya kandokando ya barabara kuu itokayo Mnarani hadi bodi ya korosho.
Mkuu wa wilaya ya Mtwara,Willman Ndile (Aliyeshika kidumu) akishiriki katika kampeni ya kufanya usafi wa mji ambapo viongozi wa siasa, watendaji wa serikali na wananchi wengine walishiriki kampeni hiyo inayofanyika kila mwisho wa wiki.
Mkuu wa wilaya ya Mtwara, Willman Ndile, akikusanya takataka tayari kwa kuzichoma moto, kama anavyoonekana hapa eneo la CRDB mjini Mtwara.
Katibu tawala wa wilaya ya Mtwara mkoani hapa, Nuru Ringo, akishiriki katika kampeni ya usafi wa mji iliyoanzishwa na mkuu wa wilaya hiyo, Willman Ndile, hapa anaonekana akizoa matawi ya miti iliyopanguliwa pembezoni mwa barabara eneo la Bima.
WILLMAN Ndile mkuu wa wilaya ya Mtwara akitupa takataka wakati aliposhiriki kwa vitendo katika kampeni ya usafi wa mji aliyoianzisha wiki iliyopita na kuendelea kila mwisho wa wiki.
MKUU wa wilaya ya Mtwara, Willman Ndile akitoa maelekezo kwa wananchi waliojitokeza kushiriki katika kampeni ya usafi ambapo pamoaja nao watendaji wa serikali,viongozi wa vyama vya siasa na viongozi wa dini walijitokeza katika kampeni hiyo inayofanyika kila mwisho wa wiki.
MKUU wa wilaya ya Mtwara Willman Kapenjama Ndile, akimwagilia mafuta biwi la takataka kabla ya kuchoma moto, wakati aliposhiriki kwa vitendo kampeni ya kufanya usafi wa mji iliyoanzishwanaye na kushirikisha wananchi wote na viongozi wa serikali na mashirika na wanasiasa wa vyama vyote.
MKUU wa wilaya ya Mtwara. Willman Kapenjama Ndile(Mwenye trakisuti) akishiriki katika kampeni ya usafi wa mji kama wanavyoonekana katika eneo la Bima mjini hapa.
MKUU wa wilaya ya Mtwara. Willman Kapenjama Ndile, akitupa taka kabla ya kuzichoma moto, wakati alipowaongoza wakazi wa Manspaa ya Mtwara Mikindani katika kampeni ya kufanya usafi wa mji iliyoanzishwa naye na kufanyika kila mwisho wa wiki.
WANANCHI wakazi wa Manspaa ya Mtwara Mikindani walioshiriki katika kufanya usafi wakiondoa magogo yaliyokuwepo kando kando ya barabara maeneo ya Bima mjini hapa jana.
KIONGOZI wa kundi maarufu la hamasa mjini Mtwara lenye makazi yake maeneo ya Mkanaledi, KWA ROHOSAFI, Bw. Shabani Store, akikata miti kwa kutumia msumeno unatumia petrol, kikundi hicho kilijitokeza katika kufanya udafi wa mazingia kwenye kampeni iliyoanzishwa na mkuu wa wilaya ya Mtwara, willman Ndile. 

Habari/Picha na Hassan Simba.

No comments: