Monday, December 30, 2013

TASWIRA MBALIMBALI ZA KUKABIDHIWA RASIMU YA KATIKA VIWANJA VYA KARIMJEE JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Rasimu ya pili ya Katiba Mpya kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba wakati wa hafla ya kukabidhiwa rasimu hiyo iliyofanyika leo kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.Rais Kikwete aliitaka Tume hiyo ya Katiba kuhakikisha kuwa Rasimu hiyo inawekwa kwenye mitandao yote ya kijamii ili wananchi waweze kuisoma na kuielewa na kuweza kutoa maoni yao kwa urahisi kupitia mitandaoni.
Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akipokea Rasimu ya pili ya Katiba Mpya kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba wakati wa hafla ya kukabidhiwa rasimu hiyo iliyofanyika leo kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rasimu hiyo kwa Makamu wa Rais,Dkt. Mohamed Gharib Bilal mara tu baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rasimu hiyo kwa Waziri Mkuu,Mh. Mizengo Pinda.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rasimu hiyo kwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,Maalim Seif Shareef Hamad.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rasimu hiyo kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,Balozi Seif Ali Idd.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rasimu hiyo Rais Mstaafu wa awamu ya Pili,Mzee Ali Hasaan Mwinyi.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rasimu hiyo kwa Waziri Mkuu Mstaafu,Mzee Cleopa Msuya.
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar,Mh. Pandu akipokea Rasimu hiyo.
Spika wa Bunge.
Jaji Mkuu.
Jaji Mkuu wa Zanzibar.
Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue.





Mwenyekiti wa Tume ya Katiba,Jaji Joseph Sinde Warioba akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya kukabidhi kwa Rais,Rasimu ya Pili ya Katiba iliyofanyika leo kwenye Viwanja vya Karimjee,jijini Dar es Salaam.Jaji Warioba alisema kuwa kulingana na idadi ya kura zilizopatikana kutoka kwa wananchi kuhusu uundwaji wa Serikali tatu, alisema kuwa idadi kubwa zaidi ni ya watu waliohitaji Serikali tatu kuliko walioipinga, hivyo Serikali tatu haipingiki ambapo kwa sasa itabaki ni kazi ya maamuzi ya Bunge la Katiba linalotarajia kuundwa mapema mwezi Januari mwakani.









No comments: